RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Jakaya Mrisho Kikwete amemteua kwa mara ya pili Mhandisi Bonaventure Baya (pichani) kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Hifadhi na Msimamizi wa Mazingira Nchini (NEMC) .

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kaimu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Tutubi Mangazeni, Mhandisi Baya atatumikia wadhifa huo kwa kipindi cha miaka mitano.

Pamoja na kuwa Mkurugenzi Mkuu wa NEMC,Mhandisi Baya pia ni Rais wa kwanza wa Baraza la Wahitimu wa Chuo Kikuu cha Ardhi na Mwenyekiti wa Kamati ya Ushauri ya Wataalamu wa Mazingira nchini.

Nyadhifa nyingine alizowahi kuzishika kabla ya uteuzi huo ni pamoja na  Mjumbe wa Bodi ya Taasisi ya Huduma ya Misitu na Mjumbe wa Bodi ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH).

Aidha Mhandisi Baya amewahi pia kuwa Mjumbe wa Bodi ya  Wizara ya Kilimo na Mjumbe wa Bodi ya Mfuko wa Hifadhi ya Misitu ya Milima ya Mashariki (TAO).

Uteuzi huo umeanza tangu Oktoba 08 mwaka 2012 ambapo Mhandisi Baya anatarajia kutumikia cheo hicho hadi mwezi  wa kumi  mwaka 2017.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...