Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Mbelwa Kairuki akiongea na Mhe. Lv Youqing, Balozi wa China hapa nchini masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Tanzania na China ikiwa ni pamoja na matarajio ya nchi hizi mbili baada ya ziara ya Rais wa China, Xi Jinping aliyoifanya hapa nchini mwezi Machi, 2013.
Balozi wa China hapa nchini Lv Youqing akifafanua jambo kwa Balozi Kairuki wakati wa mazungumzo yao.
Balozi Kairuki na Balozi Lv Youqing wakiendelea na mazungumzo huku wajumbe waliofuatana nao wakisikiliza. Kulia ni Bw. Medard Ngaiza, Afisa Mambo ya Nje kutoka Idara ya Asia na Australasia. Wengine ni Bi. Fang Wang, Afisa katika Ubalozi wa China na Bw. Lin Zhiyong (kushoto kwa Bi. Fang), Afisa Mkuu wa Ofisi ya Biashara na Uchumi ya Serikali ya China hapa nchini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...