Mh Waziri Mkuu Mizengo Pinda akitia saini kitabu cha maombolezo alipofika  mkoani Arusha leo Kuwapa pole ndugu na jamaa ambao ndugu zao wamefariki katika machimbo ya  Moramu katika eneo la Moshono Mkoani Arusha. Maporomoko hayo yametokea jana na kusababisha vifo vya watu13  na majeruhi wawili ambao mmoja ameruhusiwa na mwingine amelazwa katika Hospitali ya Mount Meru 
 Waziri Mkuu akiwa na wabunge wa Arusha na Meya pamoja na mkuu wa mkoa kwenye msiba huo mzito. Toka Kushoto ni Mbunge wa Arusha Mjini Mhe Godbless Lema, Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe Magessa Mulongo, Meya wa jiji la Arusha Mstahiki Gaudence Lyimo, Mbunge wa Arumeru Mashariki Mhe Joshua Nassari na Mbunge wa kuteuliwa Catherine Magige
 Sehemu ya majeneza ya marehemu katika ibada hiyo maalumu leo
 Kiongozi wa kidini akiombea marehemu
 Waziri Mkuu Mhe Mizengo Pinda akitoa pole kwa wafiwa





 Sehemu ya machimbo ya  Moramu iliyopotomoka na kuua watu katika eneo la Moshono Mkoani Arusha
 Waziri Mkuu Mhe Mizengo Pinda akiwa na wabunge wote wa mkoa wa Arusha na viongozi wengine akitembelea machimbo ya  Moramu katika eneo la Moshono Mkoani Arusha
 Waziri Mkuu akitembelea sehemu ya tukio
 ukaguzi ukiendelea
Waziri Mkuu akitoa maelekezo baada ya kutembelea machimbo ya  Moramu katika eneo la Moshono Mkoani Arusha. Picha zote na Chris Mfinanga

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Mungu haziweke roho za Marehemu Mahali pema peponi. Nasikitika pia na uharibufu mkubwa wa mazingira unaoonekana kwenye picha hizi.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...