Meneja wa PPF Kanda ya ziwa Meshack Bandawe akimkabidhi mifuko ya simenti Kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza Ernest Mangu, mchango wenye thamani zaidi ya shilingi milioni 2, kwaajili ya kuchangia uharakishwaji wa ujenzi wa kituo cha polisi Nyakato jijini Mwanza. 
Mwenyekiti wa kamati ya ujenzi wa kituo cha polisi Nyakato Bw. Alfred Wambura, amesema kuwa kamati yake imenuia kuhakikisha ujenzi wa kituo hicho unakamilika mwishoni mwa mwezi wa 5 na kukabidhiwa kwa jeshi la polisi.
Mikakati mingine iliyowekwa na kamati hiyo ni kukamilisha ujenzi wa nyumba ya makazi ya OSS wa Nyakato pamoja na watendaji wengine watatu wanaomfuata kwa cheo, ili kurahisisha utendaji wa kila siku wa shughuli za usalama wa jeshi hilo. 
Meneja wa PPF Kanda ya ziwa Mesharck Bandawe amesema kuwa ulinzi kwa maisha ya baadaye ya mwananchi uko ndani ya  mfuko wa uwekezaji wa PPF,  na ulinzi wa wananchi na mali zao uko chini ya jeshi la polisi hivyo amewataka wadau wengine wa mashirika mbalimbali kujitokeza kulisaidia jeshi hilo kukamilisha shughuli za utendaji kwa manufaa ya ustawi wa jamii.


Wadau wa PPF wakisikiliza kwa makini yanayojiri kwenye makabidhiano hayo.

picha na G. Sengo Blog

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...