Afisa Ubalozi  Mwandamizi Dr. Justin Seruhere  akizungumza kwa niaba ya Serikali wakati siku ya Jumatano  wiki hii Baraza Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa  lilipokuta kwa siku zima kujadili ajenda ya  Wanawake na Ulinzi na Usalama.  Tanzania  pamoja na mambo mengine ilisisitiza katika mkutano huo uwezeshwaji wa mahakama za kitaifa hususani katika nchi zenye migogoro, ili ziwe na uwezo wa kuwashitaki na kuwahukumu watuhumiwa watakaobainika kuwadhalilisha  wanawake kimapenzi. Udhalilishaji wa kimapenzi dhidi ya wanawake , watoto wa kike na hata wanaume,  ni ukatili unaoendelea kutumika kama mbinu ya vita katika nchi nyingi zenye migororo.

Na Mwandishi Maalum
Tanzania  imeungana na  mataifa mengine katika  kuendelea kukemea vitendo vya udhalilishaji wa kimapenzi  vinavyoendelea kufanyika dhidi ya wanawake, watoto na hata wanaume katika maeneo yenye migogoro.
Kwa siku nzima  ya jumatano,  Baraza Kuu la Usalama, lilikuwa na mjadala kuhusu wanawake, amani na usalama,  ambapo   wazungumzaji zaidi ya 60 waliozungumza, licha ya kukiri kwamba kumekuwa na  mafanikio fulani katika  kukabiliana na  unyanyasaji na udhalilishaji huo lakini hali  bado ni ngumu na  jitihada zaidi zilikuwa zinahitajika.
Majadiliano hayo  ambayo yamefanyika chini ya  urais wa Rwanda ambaye ndiye anayeongoza Baraza hilo kwa mwezi huu wa April, yalifunguliwa na Katibu Mkuu Ban Ki Moon  kwa kuwasilisha  Taarifa yake iliyotoa tathimini ya kina kuhusu hali ya wanawake, amani na usalama katika maeneo mbalimbali ambako migogoro bado inaendelea.
  Ujumbe wa Tanzania katika mkutano huo uliongozwa  na Dr. Justin Seruhere, Afisa Ubalozi Mwandamizi. Ambaye akizungumza kwa  akizungumza  niaba ya serikali, alisema pamoja na kuunga mkono hoja ya kufikishwa mbele ya sheria watuhumiwa wa uharamia huo, na kuongeza kasi ya kulitafutia ufumbuzi tatizo hilo,   Tanzania  pia  inasisitiza  matumizi ya   vyombo vya   kisheria  vya  ndani ya nchi husika katika kuwashughulikia watuhumiwa .
Akasema  kutokana na ukubwa wa tatizo na uyeti wake, na hasa ikizingatiwa pia kwamba  watuhumiwa hao wanatakiwa kushtakiwa  na kuhukumiwa na vyombo madhubuti,  ni vema basi vyombo hivyo vikajengewa uwezo wa kutekeleza jukumu hilo.
Hata hivyo akasema  ikidhihirika   kwamba   nchi husika   haina  vyombo imara kuifanya kazi hiyo, na kama ambavyo mara nyingi  imeshadhihirika hivyo. Basi  Tanzania inashauri  nchi husika  ziwe tayari kuwahamishia watuhumiwa hao katika vyombo vya sheria  vya kimtaifa kama vile  Mahakama ya Kimataifa ya   Makosa ya Jinai ( ICC).
Akaueleza mkutano huo kwamba vyombo hivyo vya kimataifa licha ya kasoro mbalimbali zina raslimali na  uwezo mkubwa  wa kuwashughulikiwa wahalifu.
 Akasema  Tanzania  inahimiza na kuunga  mkono hoja ya kuiongezea uwezo  ICC ili iweze kutekeleza majukumu yake na hasa ikizingatiwa kwamba kwa sasa ndicho chombo kilichopo na kinachotegemewa na jumuiya ya kimataifa.
Aidha Tanzania  katika mchango wake imesisitiza haja na umuhimu wa kuwawezesha wanawawake na watoto wa kike ili waweze kushiriki katika  masuala ya ulinzi na usalama na vilevile katika utoaji wa maamuzi  yanayohusu  uzuiaji wa migogoro  na utatuzi  wake.
Akaongeza kwamba Serikali ya Jamhuri ya  Muungano wa Tanzania inajivunia hatua yake ya kuongeza askari wanawake katika shughuli za ulinzi wa amani zinazosimamiwa na Umoja wa Mataifa ambapo  kuna askari wanaweke  200 hadi sasa . Na kwamba  Tanzania imejipanga kuongeza idadi hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...