Na Mwandishi Wetu

Tume ya Mabadiliko ya Katiba imetoa mwongozo unaoruhusu kuanza rasmi kwa uundwaji wa Mabaraza ya Katiba ya asasi, taasisi na makundi mbalimbali kwa lengo la kujadili na kutoa maoni kuhusu rasimu ya katiba inayotarajiwa kutolewa na Tume hiyo hivi karibuni.
Kwa mujibu wa mwongozo ulitolewa na Tume hiyo leo (Jumatano, 29 Mei, 2013) na kusainiwa na Mwenyekiti wa Tume hiyo Jaji Joseph Warioba, mwongozo utatumika kwa miezi mitatu kuanzia keshokutwa, Juni 1 hadi Agosti 31 mwaka huu.

“Mabaraza haya ya Katiba ya Asasi, Taasisi na Makundi ya Watu wenye malengo yanayofanana yatajadili na kutoa maoni kuhusu Rasimu ya Katiba,” amesema Jaji Warioba na kuongeza kuwa maoni hayo yanaweza kuwasilishwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba kwa njia ya randama, barua, andiko, muhtasari wa makubaliano.

Mwongozo huo, ambao utachapishwa katika magazeti mbalimbali ya siku ya Alhamisi (Mei 30, 2013) na kurudiwa tena Jumatatu (Juni 3, 2013), pia unapatikana katika tovuti mbalimbali ikiwemo ya Tume hiyo (www.katiba.go.tz) na ukurasa wa facebook wa Tume hiyo (Tume ya Mabadiliko ya Katiba Tanzania).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...