Wapenzi wetu wa Staki Shari, Tunapenda kuwafahamisha kwamba timu yenu ya Golden Bush imethibitisha
kushiriki katika Bonanza ya tarehe 19/05/2013 litakalo fanyika katika
viwanja vya Staki Shari. Golden Bush itakuja na kikosi kamili kama
kinavyoonekana katika picha hapo chini.
Golden Bush itaingia uwanjani
mnamo saa mbili kamili asubuhi tayari kutoa kipigo stahiki kwa timu
yoyote itakayopambana na sisi. Waandaaji wa mashindano wanatambua ubora
wa Golden bush itakoyokuwa ikiongozwa na nahodha wake Wisdom Ndlovu,
hivyo tunategemea kupangiwa timu itakayoonyesha upinzani na kuleta
burudani kwa mashabiki watakaokuja kushuhudia Bonanza hilo.
Tungependa kuwataarifu kwamba mchezaji wa zamani wa yanga na timu ya taifa ya Tanzania Salum Athuman Mbududu amesajiliwa rasmi baada ya kufuzu majaribio ya wiki moja, hivyo tunapenda kumtangaza kuwa kuanzia leo Salum Athuman atakuwa mchezaj halali wa Golden bush Veterans.
Imetolewa na msemaji wa timu
Onesmo Waziri "Ticotico"
Tungependa kuwataarifu kwamba mchezaji wa zamani wa yanga na timu ya taifa ya Tanzania Salum Athuman Mbududu amesajiliwa rasmi baada ya kufuzu majaribio ya wiki moja, hivyo tunapenda kumtangaza kuwa kuanzia leo Salum Athuman atakuwa mchezaj halali wa Golden bush Veterans.
Imetolewa na msemaji wa timu
Onesmo Waziri "Ticotico"
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...