Kikundi cha sarakazi cha Taifa kikishuka melini bandarini Dar es salaam kikitokea nchini China mwaka 1983 kupata mafunzo ya mchezo huo. Mwenye data za wapi walipo wataalamu hawa ambao walifanya kazi za maonesho na kuwafundisha vijana wengi, tunaomba msaada tutani...

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 18 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 10, 2013

    Hivi sasa hao wapo wapi?

    Kutokana na Ukoma na Kansa mbaya sana ya kutothamini Mchango wa Kitaaluma tiliyonayo nchini, kama uhai wao ungalipo hao wakinusurika utakuta wapo ktk Fani kama:

    1.Ufundi Baisikeli
    2.Uganga wa Kienyeji
    3.Ukaanga samaki
    4.Kuziba pancha matairi ya magari
    5.Kutumbuiza Sarakasi ktk Mabaa
    6.Wanacheza Komedi za ktk Mabaa
    7.Makondakita wa Daladala
    8.Madereva wa Bodaboda
    9.Umachinga
    10.Udalali wa vyumba na nyumba
    11.Ufundi simu kwa kutumia Kompyuta

    Hili ni janga la Taifa!

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 10, 2013

    Maoni yako nayaunga mkono ni kweli kabisa hawathaminiwi. Inawezekana kabisa wakawa wanajishughulisha na moja kati ya shughuli ulizozitaja.

    Hii sio Tanzania ya zamani kwamba hiki ni chakwetu, imebaki hiki ni changu

    Tuwe macho huko nchi inapoelekea siko

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 10, 2013

    Wewe # 1,umekulia kwenye familia yenye "Neema" hey? .Hayo makundi uliyoyataja naona kama hujayatendea haki,umeyadhalilisha.Mheshimiwa naomba ama ufute kauli yako au utoe ushahidi wa kuthibitisha madai yako.Blog ya jamii,naomba kuwasilisha.Asante


    David V

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 10, 2013

    Ankal,

    Hii haikuwa mwaka 1983 ilikuwa mapema zaidi ya hapo. Kwanini nasema hivyo?
    1. Mwaka 1983 mwendo wa 'Chou en Lai' ulikuwa ushakwisha; hata mwalimu naye hakuwa anavaa vazi hilo tena. Hii ilikuwa mapema miaka ya 70.
    2. Huyo 'kijana' aliye mbele kama sikosei anaitwa 'Rajabu.' Mwaka 1983 tayari alikuwa kiongozi kikundi cha taifa cha sarakasi. Hebu mtafute bw mmoja anaitwa Issa Sarakasi (sijui kama bado yupo idara ua Utamaduni) yeye atakuwa na data zote.

    Ahsante

    ReplyDelete
  5. AnonymousMay 10, 2013

    Ankal,

    Hii haikuwa mwaka 1983 ilikuwa mapema zaidi ya hapo. Kwanini nasema hivyo?
    1. Mwaka 1983 mwendo wa 'Chou en Lai' ulikuwa ushakwisha; hata mwalimu naye hakuwa anavaa vazi hilo tena. Hii ilikuwa mapema miaka ya 70.
    2. Huyo 'kijana' aliye mbele kama sikosei anaitwa 'Rajabu.' Mwaka 1983 tayari alikuwa kiongozi kikundi cha taifa cha sarakasi. Hebu mtafute bw mmoja anaitwa Issa Sarakasi (sijui kama bado yupo idara ua Utamaduni) yeye atakuwa na data zote.

    Ahsante

    ReplyDelete
  6. AnonymousMay 10, 2013

    Wanashuka bandarini kutokea China?! Walienda China kwa boti?

    ReplyDelete
  7. AnonymousMay 10, 2013

    Ankali naomba mwenye sanduku hama hayo hapo aniuzie niyaweke kama kumbukumbu

    ReplyDelete
  8. AnonymousMay 10, 2013

    Msemaji hapo juu hajadanganya.Maana sanaa hapa kwetu haitiliwi maanani.

    Ni kweli, watu hawa hawakuendelezwa. nakumbuka mmojawapo ni ndugu yangu alienda china kwa sanaa hiyo, sasa anachonga vinyago.Lakini anajivunia kwenda china.

    ReplyDelete
  9. AnonymousMay 10, 2013

    Wakati ule usafiri hadi China ilikuwa ni week 2

    ReplyDelete
  10. AnonymousMay 10, 2013

    safari ya kwenda china ilikuwa kwa meli duhh itakuwa imechukua miezi mingapi??

    ReplyDelete
  11. AnonymousMay 10, 2013

    umeziona chun lie...hizo

    ReplyDelete
  12. AnonymousMay 10, 2013

    Naunga mkono hoja za wadau wote hapo juu na inasikitisha sana. Tanzania hatujali wala kuthamini kazi, vipaji wala uhodari wa watu wetu kabisaaa!. Serikali haina hata mahala pa kuweka kumbukumbu na kufuatilia nyenendo za watu wake mashuhuri na hakuna hata mfuko wa kuwasaidia hili ni JANGA LA TAIFA KAMA ALIVYOSEMA MSEMAJI ALIYETANGULIA.
    Kuna siku nilikuwa pale Benjamin Mkapa Tower kwa kweli sikuamini nilipomuona JELA MTAGWA akipita pale akienda kuomba. Jamani mtu ambaye aliwekwa kwenye STAMP hakuna hata kifuta jasho? Kila STAMP iliyouzwa ilipaswa apate walau kidogo hakuna kitu jamaa anaomba nadhani alikuwa anaenda kwa DAU wa NSSF kuomba inasikitisha sana.
    Si kwenye mpira, cinema wala ngoma hakuna lolote. Mzee Morris Nyunyusa tunamkumbuka vipi? tunaenzi vipi kipaji kile?, sisi wa miaka ile tulishazoea kusikia ngoma zake tunajua taarifa ya habari hiyo amefaidika nini? Hili ni JANGA LA TAIFA, tunawakumbuka WANASIASA tu? vipaji vyetu je!
    Leonard Tenga hebu chukua changamoto hii na usaidie wachezaji wenzako wa enzi hizo usiwatupe na serikali iweke fungu iwe inasaidia wale wenye hali mbaya kiuchumi. Si wanalipa kodi wale?, hawana viinua mgongo?

    ReplyDelete
  13. AnonymousMay 10, 2013

    Kama sikosei hii haikuwa 1983 bali ni 1969 au mwanzoni mwa 70s. Kama hawa vijana wenzangu bado wapo kila mmoja atakuwa kiasi ya miaka 60.
    Nakumbuka kwenye mwaka 1965 Wachina walikuja nchini kufanya maonyesho ya biashara na utamaduni. Maonyesho yao walifanyika Mnazi mmoja kwenye uwanja wa Kidongochekundu.
    Walipoondoka wakatoa offer kwa serikali kupeleka vijana kwenda China kwa miaka 5 kujifunza fani ya sarakasi. Mimi mwenyewe nilitamani kwenda lakini kwa bahati NZURI sikuwahi kufanikiwa.

    ReplyDelete
  14. AnonymousMay 10, 2013

    DAVID V,

    Kiongozi umejibiwa Maswali yako na Anony wa: (8)
    ......................
    Msemaji hapo juu hajadanganya.Maana sanaa hapa kwetu haitiliwi maanani.

    Ni kweli, watu hawa hawakuendelezwa. nakumbuka mmojawapo ni ndugu yangu alienda china kwa sanaa hiyo, sasa anachonga vinyago.Lakini anajivunia kwenda china.
    ............................

    Na pia Anymoua wa (12)


    Naunga mkono hoja za wadau wote hapo juu na inasikitisha sana. Tanzania hatujali wala kuthamini kazi, vipaji wala uhodari wa watu wetu kabisaaa!. Serikali haina hata mahala pa kuweka kumbukumbu na kufuatilia nyenendo za watu wake mashuhuri na hakuna hata mfuko wa kuwasaidia hili ni JANGA LA TAIFA KAMA ALIVYOSEMA MSEMAJI ALIYETANGULIA.
    Kuna siku nilikuwa pale Benjamin Mkapa Tower kwa kweli sikuamini nilipomuona JELA MTAGWA akipita pale akienda kuomba. Jamani mtu ambaye aliwekwa kwenye STAMP hakuna hata kifuta jasho? Kila STAMP iliyouzwa ilipaswa apate walau kidogo hakuna kitu jamaa anaomba nadhani alikuwa anaenda kwa DAU wa NSSF kuomba inasikitisha sana.
    Si kwenye mpira, cinema wala ngoma hakuna lolote. Mzee Morris Nyunyusa tunamkumbuka vipi? tunaenzi vipi kipaji kile?, sisi wa miaka ile tulishazoea kusikia ngoma zake tunajua taarifa ya habari hiyo amefaidika nini? Hili ni JANGA LA TAIFA, tunawakumbuka WANASIASA tu? vipaji vyetu je!
    Leonard Tenga hebu chukua changamoto hii na usaidie wachezaji wenzako wa enzi hizo usiwatupe na serikali iweke fungu iwe inasaidia wale wenye hali mbaya kiuchumi. Si wanalipa kodi wale?, hawana viinua mgongo?
    ............................

    HIVYO SIFUTI KAULI YANGU, TENA NAKUONGEZEA USHAHIDI MWINGINE HAPA CHINI:

    1.Mwinga Mwanjala (Sasa anaishi Milwaukee-Marekani),
    Alikuwa Mwanariadha wa Tanzania wa Kike alipeperusha vyema Bendera ya Tanzania kwa kuleta MEDALI ZA DHAHABU na KUVUNJA REKODI mara nyingi tu.


    2.Mosi Ally (Sasa anaishi Norway),
    Alikuwa mwanariadha wa kike wa Tanzania na aliipeperusha vyema bendera ya Tanzania kwa kuleta MEDALI ZA DHAHABU na KUVUNJA REKODI nyingi tu.

    LAKINI CHA AJABU KUTOKANA NA UKOMA NA KENSA HIYO, WALIKUJA NCHINI TANZANIA KWA VIPINDI TOFAUTI WAKAENDA HADI OFISI ZA RT (RIADHA TANZANIA) ambako kwa MSHANGAO MKUBWA HAWAKUONA REKODI ZAO HATA KTK KAUNTA BOOK WALA ANGALAU DAFTARI LOLOTE LA OFISI HIZO!!!

    SASA ITAKUJA KUWA HAO WANASARAKASI?

    ReplyDelete
  15. AnonymousMay 10, 2013

    Kama nilivyoombwa,, naifuta kauli yangu, kama imeeleweka kudhalilisha baadhi ya kazi.

    ReplyDelete
  16. Je kwa taaluma walizokuwa nazo wanastahili kuomba? Tusikimbilie kusema sijui wasaidiwe..... sijui wafanyiwe hiki...!

    Jambo la msingi la kujiuliza je wale walioko kwenye fani saa hizi baada ya kuona uzoefu huo sisi tunaotoa maoni haya tuna mchango gani ili kuhakikisha wale walioko kwenye fani saa hizi hawaishii hapo Je tumejiwekea utaratibu wa kuhakikisha hali hiyo haiendelei? badala ya kuendelea kulaumu tuuuu..
    Kuendelea kulaumu hakulisaidii taifa letu jamani.

    ReplyDelete
  17. AnonymousMay 11, 2013

    TENGA, Umesikia hiyo mzee!

    ReplyDelete
  18. AnonymousMay 22, 2013

    Ilikuwa mawka 1970 ndio waliludi kutoka china na meli kwa kuwa baharini kwa siku 21, na kikundi kilivunywa na bunge la taifa mwaka 1982 wote kupelekwa mikoani na wilayani kuwa maafisa wa zaidizi wa wilaya na mkoa baada ya vyeti vyo kuja kutoka China na serikali ilishindwa kukubaliana navyo kimshaara,

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...