Na Abdulaziz,Lindi 
 Mtu mmoja alietambulika kwa jina la Ismai Mayoba(31)anaefanya kazi Bar ya Mangrove,Mkazi wa Jamhuri, Manispaa ya Lindi, amenusurika kifo baada ya kuvamiwa na kundi la Vijana waliotaka kumpora na hatimaye kumchoma moto.
Mayoba amelazwa katika Hospital ya Sokoine Mjini humo Kufuatia tukio hilo,Jeshi la Polisi wilayani Lindi limefanikiwa kumkamata mmoja kati ya watuhumiwa saba wanaosadikwia walihusika na tukio hilo lilitokea katika eneo la Mtaa wa Congo.
Akithibitisha  tukio hilo na kukamatwa kwa mtuhumiwa, Afisa Mnadhimu wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Lindi,Renatha Mzinga alimtaja Ally Manially (22) mkazi wa mtaa wa Kongo kuwa anashikiliwa na Jeshi hilo na atafikishwa mahakamani leo kujibu shitaka la kujeruhi na kujipatia pesa kwa njia ya udanganyifu ikiwa pamoja na kumchoma mwenzie Moto huku akijua ni kosa kisheria 
Aidha Mzinga alieleza kuwa Jeshi la polisi linaendelea kutafuta watuhumiwa wengine 6 waliohusika na tukio hilo Taarifa zaidi tutawaletea kuhusiana na tukio hilo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...