Ofisi ya Makamu wa Rais, kwa kupitia Programu ya Utekelezaji wa Sheria ya Usimamizi wa Mazingira (EMA-ISP) imekabidhi vitabu vinavyohusiana na Taarifa za Hali ya Mazingira na Mkakati wa Kitaifa wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi kwa Vyuo Vikuu mbalimbali hapa nchini.
Vitabu hivi ni sehemu ya Utekelezaji wa Sheria ya Usimamizi wa Mazingira katika kujenga uwezo kwa wadau kuweza kuelewa na kutunza mazingira. Ofisi kwa kupitia programu hii itaendelea kushiriana na wadau mbalimbali kuelimisha umma dhana zima ya utunzaji na uhifadhi wa mazingira hapa nchini.
 Mratibu wa Programu ya Utekelezaji wa Sheria ya Usimamizi wa Mazingira (EMAISP), Ofisi ya Makamu wa Rais, ndugu Joseph Kihaule (kushoto) akikabidhi sehemu ya vitabu hivyo kwa Mkuu wa Kitivo cha Sayansi ya Misitu na Uhifadhi ya Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine Prof. Yonika M. Nganga.

 Mratibu wa Programu ya Utekelezaji wa Sheria ya Usimamizi wa Mazingira (EMAISP), Ofisi ya Makamu wa Rais, ndugu Joseph Kihaule (kushoto) akikabidhi baadhi ya vitabu kwa Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma, Prof. Idrisa Kikula (katikati), kulia ni Prof. Kinabo akishuhudia.

 Mratibu wa Programu ya Utekelezaji wa Sheria ya Usimamizi wa Mazingira (EMAISP), Ofisi ya Makamu wa Rais, ndugu Joseph Kihaule (kulia) akikabidhi baadhi ya vitabu kwa Naibu Mrajisi wa Chuo cha Mipango na Maendeleo Vijini cha Dodoma, Prof. Innocent J.E Zilihona.


Hapa akikabidhi baadhi ya vitabu hivyo kwa  Kaimu Makamu Mkuu wa Mafunzo, ndugu Edwin Lyanda wa Chuo Kikuu cha Mkwawa, Iringa. Aidha vitabu vingine vilikabidhiwa kwa Vyuo Vikuu vya St. John’s, Dodoma, Chuo Kikuu cha Kiislamu, Morogoro na Chuo Kikuu cha St. Augustine Tawi la Morogoro (Jordan University)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...