Watanzania waishio New jersey na New York na kote kwingineko tunapenda kutoa shukurani zetu za dhati kwa ushirikiano wenu mkubwa mlio tuonyesha katika kipindi hiki kigumu. Kwa ajili ya blog za watanzania tuliweza kufikisha habari za msiba wa marehemu Adolf aka Brian aka Thadeo Lwakajende kwa watu wengi sana kwa muda mfupi sana kuliko tulivyotegemea. Kwa ushirikiano wenu huo tuliweza kufanikiwa na kuweza kukamilisha shughuli hii kwa kipindi kifupi sana kuliko tulivyokua tunafikiria.

Adolf alipelekwa kulazwa katika nyumba yake ya milele jana Jumatano May 1st, 2013 huko katika makaburi ya Mt Pleasant, Hawthorne, NY 10532.  

Tunashukuru sana sana kwa ushirikiano wenu mliotuonyesha na pia niwaombe radhi wale walioniandikia lakini sikuweza kuwajibu email zao. 

Asanteni sana,

Pauline


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 03, 2013

    RIP. Maisha lazima yaendelee, sasa hiyo mashine ya kuzikia si mletage na huku jamani. Kuzika kwa mitulinga karne hii si vema jamani.

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 07, 2013

    WATANZANIA TUJIFUNZE KUWEKA AHADI KWAMBA MAZIKO SAA FULANI BASI TUWEPO SIYO ETI LEO TUNAAMBIWA SAA FULANI AHALFU INACHUKUA LISAA LIMOJA AU LIMOJA NA NUSU NDO MNAAZA MISAA TUPO MAJU LAKINI BADO HATUBADILIKI NA ZA KIBONGO BONGO

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...