MAREHEMU MZEE JAMES
GERALD MANDAWA
Familia ya Marehemu Mzee James Gerald
Mandawa wa Kiwalani, Dar es salaam, inapenda kutoa shukurani za dhati kwenu
wote mlioshiriki kwa moyo wa upendo katika kufanikisha shughuli za msiba wa
Mzee wetu Mpendwa James Gerald Mandawa.
Tunawashukuru sana
kwa faraja na ushirikiano mkubwa mliotupatia katika kipindi hiki kigumu sana cha kuondokewa na
Baba yetu Mpenzi, ambaye tulimpumzisha katika nyumba yake ya milele huko
shambani kwake Kiluvya, Dar es salaam.
Shukurani ziwafikie Madaktari na
wauguzi wa hospitali ya Hindu Mandal, na hasa Dkt R. Kaushik , Menejimenti
na wafanyakazi wa TASAF Makao Makuu,Uongozi na wafanyakazi wa PRIDE –Arusha,
Uongozi na wafanyakazi wa DAWASCO Ilala Uongozi, wana jumuia na kwaya ya kanisa la
Kianglikana, Mt. Thomas –Yombo, majirani na marafiki wote.
Ni vigumu kuwataja wote, lakini
tunawaomba wote mpokee shukurani hizi kwa moyo mkunjufu.
“Baba,
tulikupenda sana , kuondoka kwako
kumekuwa ghafla sana , lakini
tunamshukuru Mungu kwa yote”.
Familia inapenda kuwataarifu na
kuwaomba mshiriki pamoja nasi kwenye
mkesha wa kumaliza msiba, tarehe 24 kuamkia 25 Mei, 2013- Kiwalani, na kwenye
misa ya shukurani itakayofanyika siku ya jumamosi tarehe 25 Mei, 2013 saa mbili
asubuhi, kwenye kanisa la Mt. Thomas, Yombo-Kiwalani, DSM.
BWANA ALITOA, BWANA
AMETWAA,
JINA LAKE LIHIMIDIWE
AMEN.
poleni sana familia ya mzee mandawa kwa kuondokewa na mzee wetu, mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi!!!!
ReplyDeletemagambo from canada!
jamani huyu mzee ndiye yule aliyewahi kufanyia ALAF na UNILEVER...
ReplyDeletepoleni wanafamilia