Mama Ye! leo, Mei 5, inatoa wito kwa Mh. Dk Hussein Mwinyi (MB), Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, kushughulikia kwa haraka upungufu wa idadi ya wakunga wanaohitajika ili kuwasaidia akina mama wa Tanzania kujifungua salama.

 Wakunga wana jukumu kubwa la kuwahudumia wanawake katika kipindi chote cha ujauzito na pia ni wataalamu wenye ujuzi wa kushughulikia matatizo yanayoweza kujitokeza wakati wa kujifungua. 

 Wakunga wengi wanatembea umbali mrefu na kufanya kazi masaa mengi ili watoe huduma bora kwa wanawake katika jamii zao. Wataalamu wa masuala ya afya ya wajawazito na watoto wachanga wamekadiria kuwa, iwapo wanawake wote wa Tanzania wangepata huduma za wakunga wenye ujuzi, basi maisha ya akinamama wapatao 5,000 na vichanga 32,000 yangeweza kuokolewa ifikapo 2015. 

Akiongea kwa niaba ya kampeni ya Mama Ye! Craig Ferla amesema: “Ni vyema kabisa kuwaenzi wakunga wetu katika Siku ya Wakunga Duniani. Tunapongeza ahadi za serikali kuitilia mkazo sera ya huduma za afya ya uzazi kuwa bure, lakini mengi bado yanahitaji kufanyika ili kuongeza idadi ya wahudumu wa afya.”

 Takwimu zilizochapishwa na ripoti ya Hali ya Wakunga Ulimwenguni (State of the World’s Midwives) zinaonyesha kuwa Tanzania inahitaji wakunga 9,941 zaidi ili kufikia lengo ifikapo mwaka 2015 la kuwa na asilimia 95% ya wajawazito wanaozalishwa na wahudumu wenye taaluma. 

Craig Ferla ameongeza kuwa: “Tunawaalika na kuwahimiza Watanzania kutoa shukrani kwa wakunga – na kusaidia kuwapa moyo vijana nao waamue kuwa wakunga siku za baadae. Unaweza kufanya hivyo kwa kutumia ‘Twitter’ ukiwaambia asante kwa kujituma kazini, pia waweza kuweka picha kwenye ukurasa wetu wa ‘Facebook’ zinzazowaunga mkono wakunga wetu wa Tanzania pamoja na mathalan kutambua juhudi kubwa za mkunga unayemthamini kwa kazi zake kubwa katika jamii yako.”

 Ukitaka kufahamu zaidi kuhusiana na hali ya wakunga nchini Tanzania, tembelea tovuti ya www.mamaye.or.tz/sw ambapo utapata ushahidi uliowekwa kwa namna rahisi kuelewa, habari kuhusu mashujaa katika uzazi salama, ahadi zilizowekwa na serikali na hatua mbali mbali unazoweza kuchukua web: www.mamaye.or.tz twitter: @MamaYeTZ facebook: facebook.com/MamaYeTZ 

MamaYe! 164C Msasani Beach, Kinondoni, P.O. Box 13731, Dar es Salaam, Tanzania Phone: +255 (0) 754 588 233 ili kufanikisha kampeni hii muhimu. Ipaze sauti yako isikike na toa madai ya msingi zaidi, jiunge na kampeni ya Mama Ye!

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 05, 2013

    Uzazi wa mpango unahusu! Kama tutazaa kwa uzazi wa mpango na kulimit watoto watatu kwa kila familia hata wakunga tulionao wanatosha! Uzazi wa watoto kumi kwa familia moja na kila familia ikifnaya hivi hata tufanyeje hatufikii lengo kama watanzania, mana inatkiwa propotionality yake iendaye na namba ya wazazi kwa mkunga mmoj! Hatuwezi kufika huko hata kidogo hata wakiongezeka na wanaopewa huduma waka triple haitaleta tija. Kazi za risk watu wanakwepa kusomea hayo siku hizi kwa nchi kama Tanzania ambayo hata vifaa muhimu hakuna, mzazi anatakiwa kwenda na vifaa kama pamba , gloves anapoenda kujifungua! nani akasomee ukunga? Na hata mishahara midogo na kazi zenyewe ni ngumu na zina risk nyingi. Mabadiliko yanatakiwa kuanzia mishahara yao iwe mikubwa na risk allowances zinazoeleweka, then watu wapewe elimu ya uzazi wa mpango mana mtu anazaa mpaka anazeeka hapo ni mtoto wa 15. Mungu atusaidie, kwani challenges ni nyingi mno.

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 05, 2013

    Asante mdau hapo juu. Kama ulivyosema
    1) wakunga wanakuwa at risk kupata magonjwa
    2) mshahara mdogo
    3) masaa ni mengi ya kufanya kazi
    4) Vifaa hamna
    5) wagonjwa wamekuwa wajuaji sana hadi kuwa na viburi
    6) wakunga hawapewi appreciation kwa kazi wanazofanya
    Kutokana na hizo sababu wengi hawataki kufanya kazi mawodini.
    La mwisho mkiweka limit ya umri eti mwenye 50 hatumtaki basi mnakosa wengi wenye uzoefu mkubwa wa kazi.

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 06, 2013

    Wakunga wapo Tanzania,isipokuwa ajira ndio hazipo labda.Mimi nina ndugu yangu Trained nurse midwife, amesubiri ajira ya serilkali zaidi ya miaka miwili sasa mpaka ameamua kufanya private hospital. Je do we real have midwives shortage?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...