Salaam Ankal,

Leo nimeudhiwa sana na Dereva wa Lori hili,aliekuwa ameegesha vibaya kwani alikuwa ameziba njia tena kwa makusudi kabisa,njia ambayo inaunganisha mitaa.halafu nilipomfata na kumuomba aegeshe vyema lori lake hilo ili sisi wengine tupite kwa kua njia yenyewe ni hiyo hiyo tu,alinijibu jeuri na kunitaka nifanye lolote lakini yeye hatoi gari hapo kwani ndivyo alivyoamua kupaki.kiukweli alinikera sana na kauli zake hizo,kwani alikuwa amefanya kosa kuziba njia halafu anajibu jeuri kana kwamba hii njia ni ya kwake peke yake au familia yao.

Mdau wa Globu ya Jamii.
 Hebu angalieni jamaa alivyoweka gari.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 13 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 04, 2013

    naamini kauli yako ndo iliyomfanya awe na kiburi. jifunze kuwa na kauli nzuri hata kama umekosewa

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 04, 2013

    Pole bro! Wengine huwa wanatembea na viroba kwenye hayo magari makubwa.Sasa kazi ya kiroba ikishapanda kichwani uwezo wa kufanya maamuzi ya busara hupungua sana ndio matokeo yake hayo!!!

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 04, 2013

    waendesha malori wengi wanaosafiri kwenda mikoani au nchi za nje ni wastaarabu sana sana... lakini hao wa mjini, yaani wabeba michanga, maji,wahamishaji watu, wabeba mawe, n.k ni wajeuri na hawana hata adabu! nina wasi wasi sana bangi zao huwa wanavuta ili kukomesha watu barabarani!

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 04, 2013

    Hivi na hii tutaiita barabara? Watanzania tuamke

    ReplyDelete
  5. AnonymousMay 04, 2013

    halafu michuzi na wenzako ndio mnatudanganya humu bloguni kila siku kuwa maisha tz yamekuwa mazuri hivyo sisi tulio first world turudi...kweli???maana inaonyesha kila kitu bado kipo shaghalabagala hakuna sheria, hakuna kuheshimiana, hakuna ustaarabu...jamaa hata kupiga simu polisi waje wamshughulikie huyo ameona atapoteza muda maana nothing will be done...sad story!

    mdau chicago

    ReplyDelete
  6. AnonymousMay 05, 2013

    Did you call polis?

    ReplyDelete
  7. AnonymousMay 05, 2013

    Rudi kwenu wewe! Mkataa kwao mtumwa.Ukweli ni kwamba wengi wa mnaoaoishi ughaibuni mnapiga msuli kwelikweli kuweza kujikimu tu kwa maisha ya huko.Juhudi hizo au huo msuli mngeufanyia nyumbani mngekua mbali mno!

    ReplyDelete
  8. AnonymousMay 05, 2013

    mdau wa chicago umenena la maana

    kungekua na utawala wa sheria wala hili lisingetokea....kwa wanzetu hapo angeshaamrishwa kutoa lori na fine juu na akikataa angepigwa pingu papo papo na lori kulikuta na kwenda kulikomboa kituoni kwa gharama za mwenye lori

    bado mimi sielewi kwa nini jeshi la polisi halitengenezi pesa ya nguvu kwa serikali....makosa mengi sana barabarani!

    ReplyDelete
  9. AnonymousMay 05, 2013

    Nimesikitishwa sana na kauli ya mdau wa kwanza kwani hakuna kauli yeyete inaruhusu mtu kuegesha gari hivyo...actually unahaki ya kumwita jina linalofanana na kitendo alichotenda. hii ni tabia imeenea mimi aliwahi mmoja kunitemea mate wakati najaribu kumuarifu na ninaamini nilikuwa polite. nilimpeleka police nikiwa na ushahidi wa mate na mtu tulikuwa naye ktkt gari bado police walinibeza na kudai wanavitu muhimu kufuatilia sio hilo. naungana na mdau wa hapo juu kuwa nchi haina value kabisa...... polke mdau.

    ReplyDelete
  10. AnonymousMay 05, 2013

    picha imepigwa vibaya au ni kweli sioni barabara hapo? kosa la dereva wa lorry lipo wapi sasa maana sioni barabara hapo? au ulikuwa unamaanisha amezima 'uchochoro'?
    Asante.

    ReplyDelete
  11. AnonymousMay 05, 2013

    Tuwe makini katika kutafakari mambo ukiangalia mazingira katika picha inaonyesha wazi kuwa lori lile lilikuwa pale kwa shughuli maalum ya kushusha mzigo ambapo ilibidi lisimame na kuzuia njia kwa muda na ndio maana ha ta dereva yumo garini hajashuka, ingekuwa kituko kama dereva angekuwa amekwenda maeneo yale kusalimia jamaa zake na kuegesha kama alivoegesha. ni ukosefu tu wa uvumilivu kwa aliyetuma picha na habari hii

    ReplyDelete
  12. AnonymousMay 05, 2013

    Hahahha lol pole kaka kwa kutemewa mate ! Hahahaha ! Sisi waafrica ni wanyama si binadamu kabisa

    ReplyDelete
  13. AnonymousMay 05, 2013

    hapo hamna barabara , nachoona mimi ni swimming pool .

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...