Jumuiya ya Wafanyabiashara wa Kariakoo wameahidi kuendelea kutafuta suluhu kwa njia ya mazungumzo na serikali juu ya mgogoro wa makontena ambayo yamezuiliwa bandarini, kitendo ambacho kimeathiri biashara zao kwa mda mrefu sasa kwani wemeshindwa kufanya biashara ndani na nchi jirani kwa takriban zaidi ya wiki tatu.

Tamko hili lililotolewa na Jumuiya Hii wiki iliopita, limeeleza kuwa tayari wametuma maombi kwa wizara husika na idara za serikali za mapato ili kuwepo na mkutano utakaoweza kutizama jinsi ya kutatua mgogoro wa makontena zaidi ya 400 ambayo yamezuiliwa bandarini.

Katika tamko hilo imeelezwa kuhusu dhamira yao ya kukutana na Waziri wa Fedha na Uchumi, Waziri wa Viwanda na Uwongozi wa TRA pamoja na vyombo vingine husika ili kujadili na kutafuta ufumbuzi wa kile wanachodai ni ongezeko la kodi.

Wanasisitiza kuwa kuwepo kwa pande zote hizi kwenye mkutano kutawezesha kufikia ufumbuzi.

Jambo lililopelekea kufikia uamuzi huu wa kukutana na viongozi ni kile walichokiita kutekwa nyara kwa kikao cha awali kilichofanyika na Waziri wa Fedha ambapo Chama cha Mawakala wa bandarini kilifunika nafasi hiyo kwa kujadili matatizo yao wenyewe bila ya kujali kero inayowakabili wafanyabiashara ambao tayari wameanza kupata hasara kutokana na makotena yao kukwama.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...