Na Abdulaziz Video,Lindi

Mkuu wa wilaya ya Kilwa Mkoani Lindi Abdalah Ulega amewataka viongozi na watendaji wa tarafa, kata na vijiji kushirikisha jamii katika kuzitafutia ufumbuzi kezo zinazowakabili wananchi katika mazingira yao.

 Ulega alisema kero hizo ambazo ni Upatikanaji wa huduma za kijamii pamoja na migogoro ya ardhi ambayo ikipatiwa ufumbuzi inasaidia chama cha mapinduzi kuendelea kuaminika kwa Wananchi

Ulega alitoa wito huo wakati alipokuwa anazungumza na viongozi wa serikali ya kijiji cha Mtoni wilaya humo kwenye ziara ya kuangalia miradi katika utekelezaji wa ilani ya chama cha mapinduzi

"Si vyema viongozi kuchukua uamuzi bila ya kushirikisha wananchi, badala yake matakwa ya wananchi ndiyo yatumike katika kufanya maamuzi ya kupanga mipango yote ya maendeleo na utekelezaji wake wakashirikishwa vyema kupitia vikao muhimu na vya kisheria...Alibainisha Ulega.

Mkuu huyo wa wilaya alisema hayo baada ya kutembelea zahanati ya kijiji hicho na kukuta hakuna choo cha wagonjwa na wahudumu hali ambayo ilimuuzunisha na kuwataka viongozi wa kijiji kwa kushirikiana na wananchi kuhakikisha choo hicho kinajengwa mara moja.

Aliongeza kuwa kukamilika kwa choo hicho kutapunguza usumbufu kwa wagonjwa kufika kituoni hapo kwa ajili ya kupata tiba na wauguzi wanaofanya kazi katika zanahanati hiyo.

“Ni aibu kubwa kwenye zahanati mzuri kama hii ikakosa choo kwa ajili ya wagonjwa na wahudumu hali inayotia aibu kutokana na wahudumu wa Afya badala ya kufanya kazi wanaangaikia kwenda porini kujisaidia alimaliziaUlega

Katika ziara hizo za kamati ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Kilwa wananchi walitakiwa kutambua kuwa miradi yote ya maendeleo inayotekelezwa katika vijiji vyao ni mali yao si ya serikali hivyo ni wajibu wao kuitekeleza kwa wakati na pindi ikamilikapo ikatunzwa ipasavyo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 14, 2013

    samahani kaka Michuzi nina swali linanisumbua siku nyingi naamini utanisaidia. Hivi vest si ni nguo ya ndani? Hii syle wanume mmeitoa wapi jamani?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...