Children from New Life Home in Dar es Salaam enjoy a ride on a toy train during a charity family bonanza organized by Women Footprints Initiative which provided a rare opportunity for children from orphanage centers in Dar es Salaam to play various games and music and have a chance to mingle with family members. The lively event was held at Leaders Club in the city.
  Tatu Issa from New Life Home orphanage center in Dar es Salaam get a ‘face lift’ during a charity family bonanza organized by Women Footprints Initiative which provided a rare opportunity for children from orphanage centers in Dar es Salaam to play various games and music and have a chance to mingle with family members. The lively event was held at Leaders Club in the city.

One of the children from New Life Home orphanage center in Dar es Salaam engages in jumping castle during a charity family bonanza organized by Women Footprints Initiative which provided a rare opportunity for children from orphanage centers in Dar es Salaam to play various games and music and have a chance to mingle with family members. The lively event was held at Leaders Club in the city.
 Women Footprints Initiative ( WOFI) Neema Msuya, address the media at charity family bonanza that provided a rare opportunity for children from orphanage centers in Dar es Salaam to play various games and music and have a chance to mingle with family members. The lively event was held at Leaders Club in the city.
 ============  ============  ==========


Watoto yatima washiriki tamasha la hisani la WoFI.

Dar es Salaam Mei 4, 2013: Shirika la Women Footprints Initiative (WoFI), leo limefanya tamasha la hisani la familia lijulikanalo kama Cheza Time na kushirikisha watoto kutoka vituo vya kulelea watoto yatima ambao wamecheza michezo mbalimbali na kupata fursa ya kujumuika na ndugu zao. Tukio hilo la aina yake limefanyika katika viwanja vya Leaders Club.  

Meneja miradi wa WoFI Neema N. Msuya amesema kuwa pamoja na kutoa burudani za michezo, tamasha hilo pia limetumika kupata fedha za kusaidia vituo hivyo vya watoto yatima na kuendeleza miradi ya wanawake inayoendeshwa na shirika hilo kwa lengo la kusaidia watoto na kuwawezesha kina mama kiuchumi..  

Alisema kuwa kusudi kubwa ya shirika la WoFI ni kuwawezesha watoto hao kupata mahitaji yao ya msingi ikiwa ni pamoja na kuwapatia elimu na kuyataka makampuni, mashirika na watu binafsi kujitokeza kusaidia ili kuwajengea watoto hao msingi imara wa maisha yao ya baadaye.

“Tamasha  la hisani la familia tunalofanya hapa leo linakusudiwa kuwa tukio la kila mwaka ambalo, mbali ya kuhamasisha wahisani kuchangia mfuko wa shirika, litatumika kama chombo cha kuwaunganisha watoto na ndugu na jamaa zao huku wakiburudika na vinywaji baridi, michezo mbalimbali pamoja na kucheza muziki”, alisema.

Tamasha la leo lililovuta hisia za watu mbalimbali lilishuhudia watoto wachangamfu wakishiriki michezo ikiwa ni pamoja na mpira wa miguu, kuruka, kuogolea na kukimbia ndani ya gunia. Watoto hao pia walipata fursa ya kuonyesha vipaji vyao vya kuimba na kucheza muziki.

Shirika la WoFI ambalo siyo la kibiashara vile vile huendesha kampeni ya kuwaelimisha wasichana walioacha shule kwa sababu mbalimbali kuachana na tabia hatarishi na kujishughulisha na biashara halali ili kujipatia kipato cha kuwasaidia katika maisha yao. Kampeni hii inafahamika kama Binti Amka.

Kampeni nyingine inayoendeshwa na shirika hili inajulikana kama Jitambue uwezo wako Sasa ambayo inawahamasisha wasichana wa shule za sekondari kusoma kwa bidii na kushinda vishawishi vilivyo mbele yao na hatimaye kutimiza ndoto za kuwa na maisha bora hapo baadaye. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 05, 2013

    Asante sana dada Neema kwa Moyo huo wa kuwasaidia hawa watoto waweze kutimiza ndoto zao.Kama una internet naomba uwawekee huu wimbo wa Brenda Fassie-Ag Shame Lovey(a.k.a Mi -do-do-do-do-do-laa-doo-tiiii) uwaburudishe na kuwapa mazoezi.Wimbo ulirekodiwa kama miaka 25 hivi iliyopita lakini mzuri sana kwa Watoto.

    http://www.youtube.com/watch?v=ocmywGu5LY4

    David V

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 07, 2013

    Asante dada neema kwa kuwasaidia hawa watoto mungu atakulipa kwa wema wako lakin jamani kuwachora michoro ya kishetani spider sijui nini na nini tuiache jamani najua hamuwezi kunielewa nisemacho lakin taifa la kiafrica kitanzania nilapotea tusipoangalia kwa kizazi chetu kuwalea maadili mema hawa watoto wetu sio kukopi kila kitu kilichopo huko majuu tafadhalini ndugu zangu tuangaliye sana jambo hili

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...