Waziri Mkuu Pinda akizungumza kwenye viwanja vya Nyerere Skwea,mara baada ya kupokea matembezi ya mshikamano yaliyowajumuisha wasanii wa muziki wa kizazi kipya/Filamu pamoja na wadau wengine wa sanaaa mbalimbali bila kuwasahau Clouds FM ambao ndio walioratibu shughuli nzima ya matembezi hayo yakiwa na lengo la kuiomba serikali iendelee kuzilinda fursa zilizopo na ikibidi kuziongeza katika wigo mpana ili kukwamua maisha ya wasanii na vijana walioko katika nyanja mbalimbali,kama vile haitoshi matembezi hayo yalikuwa na ujumbe uliolenga kupinga uharamia wa kazi za sanaa hapa nchini.Aidha Clouds FM pia walizindua msimu wao mpya uliopewa jina la MADE  IN TANZANIA ndani yake kukiwa na kampeni kubwa ya TWENZETU katika harakati ya kuihamasisha jamii kujivunia vya kwao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 13, 2013

    Mie siku zote sielewi kilio hichi cha wana sanaa, sio bongo tu, kutaka serikali iwalindie mali yao. Ni kama mimi nikitaka serikali inilindie shamba langu. Nakubali kuwa wizi wa kazi zao si kitu kizuri, nisichoelewa ni kwa nini sisi sote tulipie ulinzi wa njia zao za kukusanya utajiri wao, na angalia hivi baina yao ni matajiri kweli.Serikali iweke kodi maalum ya wasanii hawa ili iunde kikosi maalum cha kuchunga mashamba yao, siyo kutumia mfuko wa wananchi.
    Wakatabahu

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 13, 2013

    Mbona mie sijaelewa nini? kilicho nyuma ya mradi huu,maana naona kama ni wasanii kuibiwa kazi zao,sio kuwa
    vyombo na wausika wote kuwa wameshirikiana au kushirikishwa katika hili,naona baadhi ya wasanii wa kizazi kipya tu na Clouds media ndio wapo mbele,sasa BASATA wapo wapi? Wizara ya Habari,michezo na utamaduni ipo wapi haina mwakilishi?
    Bendi za taarabu na muziki wa dansi hazionekani hapa! wachekeshaji nao wamesusia harakati hizi au?
    Kweli vita hivi vitakua na ushindi?
    au labda Ruge na timu yake wanataka kuwanyang'anya vijiti wenzao kwa kujifanya wao ndio wenye uchungu na sanaa,mbona kampeni hii imekuwa kama mchezo wa kuigiza

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...