Katibu wa NEC ya CCM, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro, akimlaki Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Ukombozi wa Palestina (PLO), Tayaseer Khalid ambaye pia ni mjube wa Halmashauri Kuu ya Chama hicho, alipowasili asubuhi hii, Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam kwa ajili ya ziara ya Kichama, hapa nchini. Pamoja naye ni Wajumbe wa NEC wa PLO, Jehad Zneed na Saleh Raafat.
 Katibu wa NEC ya CCM, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro, akiwa na Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Ukombozi wa Palestina (PLO), Tayaseer Khalid ambaye pia ni mjube wa Halmashauri Kuu ya Chama hicho, alipowasili asubuhi hii, Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julisu Nyerere, jijini Dar es Salaam kwa ajili ya ziara ya Kichama, hapa nchini. Pamoja naye ni Wajumbe wa NEC wa PLO, Jehad Zneed na Saleh Raafat (Kushoto). Wapili kulia ni Balozi wa Palestina hapa nchini  Dk. Nasri Abujasir.
Katibu wa NEC ya CCM, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro, akizingumza Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Ukombozi wa Palestina (PLO), Tayaseer Khalid ambaye pia ni mjube wa Halmashauri Kuu ya Chama hicho, kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam. Kiongozi huyo anatarajiwa kuwa na mazungumzo na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana kuanzia saa 3.30 asubuhi hii, kwenye hoteli ya Protea Courtyard, jijini Dar es Salaam. PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 8 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 12, 2013

    Hivi kweli huyo mmoja wa wageni toka Palestina (Mdada) ndiyo kavaa t-shirt imeandikwa ''KISS ME STUPID'' au macho yangu!?

    Hivi wana wachukuliaje chama cha CCM1? Wenyeji wao kwa ujumla!?

    Ningekuwa mimi ni Asha Migiro sijui ningesema nimepata dharura rais kaniita hivyo nimwache dereva tu au lah!

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 12, 2013

    Hiyo ze-fulanaz ya huyo mama kwenye huo msafara nimeipenda

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 12, 2013

    maskini mama wa watu...kavaa T-shirt imeandikwa " Kiis me... Stupid"?...

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 12, 2013

    Sasa huyo huko nyuma alovaa T shirt yenye maneno Kiss Me Stupid aliingiajeVIP loune? Jamani asiogopwe mtu! Aaambiwe hapa kwetu huingii, basi.

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 12, 2013

    Wanawake woooooote Tanzania tungekuwa tunajiamini kama huyu mama hakika tungefika mbali sana, hata maendelea yange kuwa makubwa. Kwanza anafanya mazoezi sana kila siku siunaona mwili wake ulivyo fiti, na pia ana jiheshimu na kujiamini kiasi kikubwa sana. Wanawake tumuige jamani, tuige busara yake, hekima na ukakamavu wake.

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 12, 2013

    Mh MNEC wa Palestina Amevaa Tshirt inasomekaje? KISS ME 26......

    ReplyDelete
  7. AnonymousJune 12, 2013

    Nini tatizo??ili mradi amejisitiri hakuja uchi, nakumbuka enzi zile za miaka ya themanini na tisini ya mwanzo wabongo wengi tulikua tunavaa fulana zenye maneno makali pengine zaidi ya haya tuyaonayo kwa huyu mgeni wetu, lakini kwakua hutukujua na hatukua na njia mbadala ilitulazimu tujitukanishe mbele za watu.Hapa naongelea enzi zile za DABWADA AU KILAKA, nguo ikitoboka hakuna kutupa ni kubandika kilaka tu ngoma mdundo na ajabu zaidi ilikua rangi ya kilaka haiendani na rangi ya nguo asilia,utakuta kilaka rangi nyekundu na nguo asilia rangi nyeupe.

    ReplyDelete
  8. AnonymousJune 12, 2013

    Hiyo mbaya sana!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...