Daladala moja inayofanya Safari zake kati ya Gongolamboto - Masaki imetumbukia mtaroni mapema leo asubuhi maeneo ya Magomeni Mikumi jijini Dar es Salaam,baada ya kutaka kuovertake gari ndogo aina ya Noah hali iliyopelekea kupoteza muelekeo kwa daladala hilo na kuingia mtaroni lakini kwa bahati nzuri hakuna aliyepoteza maisha na watu kadhaa walijeruhiwa.
Askari Polisi wakiangalia ajali hiyo wakati walipofika kuangalia.
Askari Polisi akichukua maelezo ya baadhi ya abiria walikuwepo kwenye Daladala hilo,ambao waliumia baada ya kuingia Mtaroni.
Break Down ikinyanyua Daladala hilo.Picha na Mdau Krantz Mwantepele.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. Bange mbaya jamani! Sumatra mpo na mnaona wavuta bange wenu?

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 03, 2013

    Hiyo mitaro ifunikwe sasa. Yaani,watu kibao wanakufa na hiyo mishomo. Jamani, Mkitengeneza Barabara, mue mnaweka na bajeti ya kufunika mitaro. Watu wazitumie hizo njia ziwe za kutembelea, kama walivyo fanya kisutu. Yaani, mtu hata huwezi kukwepa ajali, cause utatumbukia kwenye Mtaro.

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 03, 2013

    Nakubaliana na wewe mdau. Wavuta bangi wengi ndo hao hao madereva mabarabarani! unakuta mtu yuko kwenye msikano wakati hata leseni hana.

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 03, 2013

    Duh! hii 109 ndio itavuta hiyo daladala?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...