Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini, John Casmir Minja akimvisha cheo cha Mkaguzi wa Magereza Mwanafunzi Na. 2623 S/SGT Clementina Nzunda kwa niaba ya wahitimu wanzake 51 ambapo wametunukiwa cheo hicho tangu leo tarehe 10 Juni, 2013. Sherehe hizo zimefanyika leo katika viwanja vya Chuo cha Udereva na Ufundi Kingolwira, Morogoro.
Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini, John Casmir Minja akimvisha cheo cha Mkaguzi Msaidizi wa Magereza Mwanafunzi Na 2623 S/SGT Clementina Nzunda kwa niaba ya Wahitimu waliomaliza Mafunzo ya Uongozi Daraja la Pili katika Chuo cha Udereva na Ufundi Kingolwira, Morogoro.
Wahitimu wa Kozi ya Uongozi daraja la pili Kozi Namba 1 ya Mwaka 2013 wakiwa katika mwendo wa pole wakijiandaa kutoa heshima mbele ya Mgeni rasmi Kamishna Jenerali wa Magereza, John Casmir Minja hayupo pichani. Sherehe hizo zimefanyika leo katika Chuo cha Udereva na Ufundi Kingolwira, Morogoro.
Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini, John Casmir Minja akisikiliza Risala ya wahitimu wa Mafunzo ya Uongozi daraja la Pili na Kozi ya Ukuu wa Kambi(RSM) hawapo pichani leo katika Chuo cha Udereva na Ufundi Kingolwira, Morogoro.
Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini, John Casmir Minja (aliyeko katikati) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wahitimu wa Kozi ya Uongozi daraja la pili na Kozi ya Ukuu wa Kambi(RSM) Mara tu baada ya kufunga Mafunzo hayo leo katika Chuo cha Udereva na Ufundi Kingolwira, Morogoro.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 11, 2013

    Inaonekana huu ni msimu wa kupandishana vyoe kwa hawa jamaa. Lakini Hongereni labda lipo la maana munalolifanya.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...