Na Abdulaziz Video,Lindi

Timu ya Karikoo Fc ya mjini lindi Ilishuka dimbani kumenyana na timu ya Abajalo Fc ya mjini Dar es salaam Kipute hicho kilichopigwa katika dimba la ILULU uwanja ambao una historia ya kutoiruhusu timu ngeni kuondoka na ushindi.

Mpira ulianza kwa kasi kwa timu zote kushambuliana kwa kasi, kadri muda ulivyokuwa ukisogea Abajalo Fc walionekana kuutawala mchezo huo kwa kuweza kufika langoni mwa Kariakoo Fc mara nyingi lakini ngome ya Kariakoo FC ilikuwa imara, hada mapumziko timu zilikwa bila kwa bila.


Kipindi cha pili kilianza kwa timu ya kariakoo kuliandama lango la Abajalo na kuweza kupata penalt ambayo haikuzaa matunda baada ya Nahodha wa Timu ya Kariakoo Anafy Jamvi kushindwa kuiwezesha timu yake kuongoza kutokana na kupiga penalti hiyo kwa madaha na mpira kwenda nje.

Dakika chache baada ya kukosekana kwa penalti hiyo Kariakoo iliongeza kasi na kuliandama kwa mfululizo lango la Abajalo na Mchezaji Muhsin ndiye aliwainua mashabiki mara baada ya kufunga goli maridadi kwa kupokea mpira wa cross uliopigwa na salum abdalah naye kupiga kichwa maridadi na kutinga wavuni goli ambalo Hadi mwisho wa mchezo matokeo yalibakia KARIAKOO LINDI 1-0 ABAJALO FC.

(Agg 3-2.), Matokeo ambayo ambayo yameivusha timu ya Kariakoo na kujijengea matumiani ya Kurudi Ligi kuu Ya Tanzania Bara Katika mchezo wa kwanza uliofanyika mwishoni mwa wiki timu ya kariakoo ilitoka sare ya mabao 2-2 mchezo uliochezwa jijini Dar es salaam na kwa matokeo hayo kariakoo imefanikiwa kusonga mbele katika hatua ya 3, ambapo itacheza na mshindi kati ya FRANCE RANGERS (Dar) au AFRICAN SPORTS (Tanga)
Mtanange ukiendelea
Furaha ya ushindi
Nyomi la Mashabiki.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...