Mwenyekiti wa chama kikuu cha ushirika mkoa wa Kilimanjaro(KNCU)Maynad Swai akitoa taarifa kwenye mkutano mkuu wa chama hicho unaofanyika katika ukumbi wa Hotel ya KNCU ulioo mjini Moshi.
Kaimu mrajisi wa vyama vya ushirika nchini Bw Peter Rutabanzibwa akizungumza katika mkutano mkuu wa chama cha ushirika mkoa wa Kilimanjaro KNCU.
Wajumbe wa mkutano mkuu wa chama kikuu cha ushirika mkoa wa Kilimanjaro wakifuatilia kwa makini maelezo ya mwenyekiti(hayupo pichani).
Mjumbe akichangia hoja katika mkutano huo.
Baadhi ya vingozi wa KNCU katika mkutano huo.

Na Dixon Busagaga wa globu ya jamii Moshi

Serikali inawasiliana na benki kuu ili kuweka mipango madhubuti ya kuziimarisha na kuziendeleza benki za ushirika nchini ili kuzijengea uwezo wa kuwahudumia wakulima kwa kuvipa mikopo vyama vikuu vya ushirika badala ya kuzitegemea taasisi nyingine za fedha.

Kaimu mrajisi wa vyama vya ushirika nchini Bw Peter Rutabanzibwa amesema hayo katika mkutano mkuu wa chama kikuu cha ushirika mkoani kilimanjaro (KNCU) baada ya wajumbe wake kueleza kutoridhiswha kwake na utendaji wa benki ya ushirika mkoani humo ya kilimanjaro co-operative bank(KCBL).

Bw Rutabanzibwa amesema, lengo la serikali ni kuhakikisha kuwa benki hizo ikiwemo ya kilimanjaro zinafikiwa kiwango cha juu katika kuwahudumia wakulima hivyo jukumu la wanachama wa vyama vyote vya ushirika nchini na kuziunga mkono benki hizo.

Hata hivyo baadhi ya wajumbe wa mkutano huo walieleza kutoridhishwa kwao na mwenendo wa benki hiyo ambayo imekuwa ikifanya semina za kuvishawishi vyama vya msingi vya ushirika vijitenge na kncu katika biashara ya kahawa na kuuvuruga ushirika.

Kutokana na hali hiyo mwenyekiti wa KNCU Bw Maynard Swai ameutaka mkutano huo utoe tamko juu ya benki hiyo kutaka kuusambaratisha ushirika na kupendekeza wajumbe wawili wa bodi ya wakurugenzi wa KNCU waingie kwenye bodi ya wakurugenzi ya benki hiyo ili kudhiti hali hiyo.

Katika taarifa yake mwenyekiti wa kncu Bw Swai amesema, chama hicho kimeimarisha mtaji wa benki hiyo kwa kuipatia zaidi ya shs. 153.6mil/= kutokana na kilo 1,536,340 za kahawa iliyokusanywa kutoka vyama vya msingi vya ushirika na kuuzwa kwa msimu wa 2009/2010.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 29, 2013

    KNCU!

    Kwa anguko la kilimo cha kahawa mkoani Kilimanjaro,KNCU inajivunia lipi?

    Je mna mikakati gani ya kufufua zao hili? ama nguvu zaidi sasa ziko ktk benki na hiyo hospitali ya rufaa mnayotaka kuanzisha.
    Shame on you KNCU!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...