Mshindi wa shindano la BE FORWARD PHOTO CONTEST ambaye ni mwanafunzi wa chuo kikuu cha Makerere nchini Uganda,Bwa.Sunday Robert akifanya mahojiano mafupi mbele ya wanahabari kutoka vyombo mbalimbali,namna alivyojishindia gari aina ya Landcruiser Prado kupitia shindano hilo la mtandao wa kijamii wa facebook.
Meneja mauzo  wa kampuni ya BE FORWARD .JP ambao ni wasafirishaji wa magari kutoka Japan kwenda nchi mbalimbali,Bwa.Eiichi Mizuyama akimkabidhi Bwa.Sunday Robert mfano wa funguo mara baada ya kujishindia gari aina ya   Landcruiser Prado kupitia shindano hilo la  BE FORWARD PHOTO CONTEST lililofanyika kwa njia ya Mtandao wa kijamii wa facebook.

Bwa. Eiichi Mizuyama alisema kuwa pamoja na kumpata mshindi huyo wataendelea kufanya shindano hilo na kuwapata washindi wengine,katika suala zima la kuhakikisha kampuni hiyo ya BE FORWARD .JP inaendelea kuwajali wateja wake kwa namna mbalimbali,ikiwemo na suala la zima la umakini mkubwa katika kusafirisha bidhaa zao zikiwa salama mpaka mlangoni kwa mteja wao.

Bwa. Eiichi ameeleza kuwa pamoja na kuwa kampuni hiyo makao yake yako Japan,lakini pia wamefungua tawi la kampuni hiyo hapa nchini katika suala zima la kuwahudumia wateja watakaokuwa wanahitaji huduma zao za uhakika.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 10 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 08, 2013

    JAMANI, JAMANI, SIO MAKELELE; NI MAKERERE!

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 08, 2013

    Dah, waandishi wa hii blog jamani hata kuandika MAKERERE imekuwa taabu? Haileti picha nzuri kushindwa hata kuandika jina la mahali sawasawa. Siyo MAKELELE jamani...

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 08, 2013

    Duuh, ama kweli Kiswahili kimekwisha....
    Makelele ndio wapi tena??
    Jamani kazeni ulimi. Matamshi ya "R" mbona mtihani Bongo siku hizi??
    Ni Chuo cha MAKERERE.....

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 08, 2013

    Jamani ni Makerere

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 08, 2013

    Ni Makerere

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 08, 2013

    This is getting a bit stupid, ? Makelele, what????????, it should be MAKERERE, Michuzi ajiri watu wenye alau kadiploma ka uandishi wa habari,unajiaribia jina kwa uandishi huu uchwala!

    ReplyDelete
    Replies
    1. AnonymousJune 09, 2013

      Na wewe Pia, siyo uchwala ni uchwara

      Delete
    2. AnonymousJune 09, 2013

      Na wewe Pia, siyo uchwala ni uchwara

      Delete
  7. AnonymousJune 09, 2013

    Makelele?au Makerere?

    ReplyDelete
  8. AnonymousJune 09, 2013

    JAMANI WATANZANIA WENZETU??????????MBONA MNAHARIBU KISWAHILI?WHAT THE MEANING OF MAKELELE?NI MAKERERE PLEASE.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...