Lt. Jenerali Paul Ignace Mella,Mkuu Mpya wa Jeshi la Mseto kati ya Umoja wa Mataifa na Umoja wa Afrika maarufu kama UNAMID linalolinda Amani huko DARFUR Nchini Sudan. Lt. Jenerali. Mella kutoka Jeshi la Wananchi wa Tanzania ( JWTZ) anachukua nafasi iliyoachwa na Lt. Jenerali Patrick Nyamvumba kutoka Rwanda ambaye amemaliza muda wake Machi 31,2013.

Kwa mara nyingine Bendera ya Tanzania imeendelea kupepea katika Tasnia ya Ulinzi wa Amani ya Kimataifa.

Mapema wiki hii, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon na Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika Bi. Nkosizana Dlamin Zuma wametangaza uteuzi wa Luteni General Paul Ignace Mella Kutoka Jeshi la Wananchi wa Tanzania ( JWTZ) kuwa Mkuu Mpya wa Jeshi la Kulinda Amani la Umoja wa Mataifa huko Darfur ( UNAMID)

Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon, na nakala yake kutumwa katika Uwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, imeeleza kwamba, Lt. Gen. Mella anachukua nafasi iliyoachwa na Mkuu wa zamani wa Jeshi hilo (UNAMID), Lt. Gen Patrick Nyamvumba kutoka Rwanda ambaye amemaliza muda wake wa utumishi March 31,2013.

Wasifu wa Luteni General Paul Ignace Mella unaelezwa kuwa ni Mwanajeshi wa muda mrefu na mwenye uzoefu na utumishi uliotukuka katika JWTZ akiwa amewahi kushika nyadhifa mbali mbali muhimu za uongozi.

Baadhi ya nyadhifa hizo ni pamoja na Naibu Kamanda Kikosi cha Tanzania chini ya Umoja wa Mataifa huko Liberia ( 1993-95), Kamanda wa Kikosi cha JWTZ, Afisa Mnadhimu-Makao Makuu ya Jeshi, Mwambata Jeshi-Ubalozi wa Tanzania Uganda na hadi sasa alikuwa ni Mkuu wa Usalama na Utambuzi- JWTZ.

Uteuzi wa Lt. Generali Mella unafuatia mchakato mrefu ulioshindanisha wateuliwa kutoka nchi mbalimbali duniani, na hatimaye yeyé akaibuka mshindi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 06, 2013

    Hongera sana Jenerali kwa kuchaguliwa kwako kuongoza jeshi la kulinda amani.
    Emmanuel.

    ReplyDelete
  2. Hongera sana, duh! si mchezo kwenye mchakato hadi unachagulia sio siri unakuwa umestahili,

    Cesc Henry Sn.

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 06, 2013

    HONGERA SANA UNCLE MELA, MUNGU AKULINDE.

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 07, 2013

    Hongera sana ukitumika kwa bidii na kwa uaminifu Mungu hakuachi kamwe Hongera!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...