Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimfariji Msanii wa taarabu Hadija Koppa nyumbani kwake mjini Bagamoyo jana kufuatia kifo cha Mumwewe Marehemu Jaffari Ali Yusuf aliyefariki na kuzikwa wiki iliyopita.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiifariji familia na ndugu jamaa wa msanii maarufu wa taarabu na mjumbe wa Halmashauri kuu taifa CCM  Hadija Koppa kufuatia  kifo cha mumwewe Jaffari Ali Yusuf kilichotokea wiki iliyopita na kuzikwa jijini Dar es Salaam.Wa pili kushoto ni Waziri wa Elimu Dkt Shukuru Kawambwa na wa pili kulia  ni Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo  Mhe. Ahmed Kipozi na kulia ni mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa CCM Ndugu Ridhwani Kikwete. Picha na Freddy Maro

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 09, 2013

    Mh. Ahmed Kipozi! ni yule aliyekuwa mtangazaji?

    Ohh, sasa ngoja nami nijipange walau awamu ijayo "Nilambe hizi post"

    Poleni kwa msiba.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 09, 2013

    ndiye huyu huyu kipozi unayemfahamu.Ila jipange maana kuna katiba mpya inakuja na pia raisi ajaye si mtu wa huruma huruma za kuwapa watu madaraka.

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 09, 2013

    Ahmed Kipozi ndio huyo huyo wa RTD.

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 10, 2013

    Jamani mimi tangu nakua namsikia Hadija KoPA, yaani miaka yote hiyo ya uimbaji ndo nyumba yake iko hivyo!!! jama ni kwa kinara km huyo alitakiwa kuwa na mansion. Mh kama mambo ndo hivyo ni bora kufanya kazi zingine na sio uimbaji/usanii Africa, loh!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...