ADELAIDA JOHN KWALEWELE MIKONGOTI (BINTI KWALE)
Familia ya Marehemu Pius Hassan Ngavochya Mikongoti
ya Dar Es Salaam inapenda kutoa shukrani za dhati kwa kutufariji katika
msiba mkubwa tulioupata kwenye familia kwa kuondokewa na Mama Yetu
kipenzi Adelaida John Kwarewele Mikongoti (Bint Kware) mnamo tarehe 27th May 2013 huko Mlimba Ifakara Morogoro na kuzikwa huko Kijijini Mlimba Ifakara Morogoro.
Sio rahisi kumshukuru kila mmoja lakini kwa namna ya
pekee tunapenda kutoa Shukrani zetu za dhati kwa Kaimu Baba Askofu Mkuu
wa Jimbo kuu la Mahenge Father Mcharange kwa kushiriki nasi kwenye misa
mpaka maziko ya Mpendwa mama yetu, Pia twamshukuru kwa namna ya pekee
Paroko wa Parokia ya Mlimba kwa kuwa nasi karibu siku zote tangu kuumwa
mpaka siku ya mazishi ya kipenzi mama yetu, Twamshukuru pia Mchungaji
Mwasongwe wa Kanisa la Moraviana Mabibo Dar es salaam na Mchungaji na
waumini wa wa Moravian Kanisa la Mlimba na Uongozi wa Msikiti Mkuu wa
Mlimba – Ifakara.
Vile vile familia kwa namna ya pekee inapenda
kuwashukuru Madaktari na Wafanyakazi wa Tumaini Hospital, Regency na
Aghakhan na Hospitali ya Mlimba ambako marehemu alikuwa akitibiwa kwa
matatizo yake ya kisukari, Pia Familia inatoa shukrani za dhati kwa
Uongozi wa wafanyakazi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, Uongozi na
Wafanyakazi wa Rufiji River Basin Iringa, Uongozi na wafanyakazi wa
Tanesco Kigamboni-DSM na Mlimba Kihansi, Uongozi na Wafanyakazi wa GS1
Tanzania, Idara ya Uhamiaji Makao Makuu – Wizara ya Mambo ya Ndani ya
nchi, Uongozi wa Nakiete Pharmacy, Brons Investments, Pia kwa namna ya
kipee tunawashukuru Mr. Tamim Lukuta kwa niaba ya Friends of Mlimba,
Zebby Kipussy na wengineo ambao walikwenda nasi mpaka Mlimba kuanzia
siku ya kwanza mpaka siku ya mwisho, Bila kuwasahau Marafiki wa Mrs
Baldwina Msomba na waumini wa Kanisa la Moravian Mabibo, Marafiki,
Majirani wa Dar Es Salaam, Mlimba, na kwingineko ambao waliguswa na
matatizo yetu na kwa namna ya kipekee kutufariji na kuwa nasi mpaka
kijijini Mlimba.
Marafiki, jamaa na watakia heri wote waliokuwa
wakitufariji kwa simu, kwa meseji kiukweli familia imefarijika sana na
sisi kama familia hatuna cha kuwalipa ila tunawaweka kwenye sala zetu
kwani mmetuachia deni.
Misa ya arobaini ya Kumuombea Marehemu itafanyika Kijijini Mlimba tarehe 12 kuamkia 13 Julai 2013.
Bwana Ametoa, Bwana Ametwaa Jina la Bwana Lihimidiwe.
Raha ya Milele Umpe Eeeh Bwana …. Na Mwanga wa Milele Umuangazie. Apumzike kwa Amani – Amina.
Wapendwa: Eugene, Baldwina (Lake) na ndugu wote, poleni sana kwa msiba huu wa kuondokewa na mama yetu mpendwa. Wakati huu wa majonzi Roho wa Mungu awatie nguvu na awape faraja sawasawa na kadili ya mapenzi yake.
ReplyDeleteYeye aliyemtwaa na atampumzisha kwa amani ya milele, mpaka tutakapoonana nae tena maana aliahidi hivyo.
Amina.
Robert, CA