Meza kuu wakati wa hafla hiyo
Spika wa bunge Anne Makinda akizungumza katika hafla ya kumuaga Spika Mstaafu Samuel Sitta kwenye viwanja vya bunge Mjini Dodoma juni 21, 2013.
Mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda akisalimiana na Mheshimiwa Dr. Maua Daftari ambaye alikuwa ni Mwenyekiti wa Kamati ya hafla ya kumuaga Spika wa zamani,Mh. Samuel Sitta kwenye viwanja vya Bunge Mjini Dodoma Juni 21, 2013.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza kabla ya kukabidhi zawadi zake pichani kwa Spika mstaafu. Samuel Sitta katika hafla ya kumuaga Spika huyo kwenye viwanja vya Bunge Mjini Dodoma Juni 21, 2013.Kushoto kwake ni mkewe Tunu na wengine kutoka kulia ni Mke wa Spika wa Zamani Margareth Sitta, Spika wa zamani Samuel Sitta na Spika wa Bunge Anne Makinda. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 8 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 22, 2013

    Hii mpya. Miaka mingapi imepita?

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 22, 2013

    Anaagwa kwani anaacha ubunge?

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 22, 2013

    Really?? Now?? Its like wishing a happy b'day months later,,,c'on,,,They could make a better use of that money.

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 22, 2013

    Next President Kwa hivyo lazima Waheshimiwa wampe heshima yake ndio kumuweka sawa. Amefanya mabadiliko kwenye bunge kwa kiasi kikubwa sana. Tumpeni pongezi zake. Mimi Mhe Sitta naona kwa mara ya kwanza Nchi yetu watu watapiga kura kwa kutofuata Itikadi zao kama Mhe Sitta atakuwa Mgombea wa Uraisi Kupitia Chama Cha Mapinduzi.

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 23, 2013

    Huyo aliyekuambia ana gombea Urais ni nani? au una ota ndoto za kimweri? Mie sitaki kuona wazee wastaafu kujitekeza tokeza kwenye kugombea high positions. once umestaafu please take time to stay home and enjoy life with your family. halafu mie naona sasa hivi tuwaachie vijani hii nchi jamani, labda mabadiliko yatatokea haraka haraka, we so need a lot of changes in Tanzania. Tumechoka sana na mambo yale yale, sera zile zile, misemo ile ile......

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 23, 2013

    Na makatibu wakuu wastaafu wa miaka yooote walikuwapo

    ReplyDelete
  7. AnonymousJune 23, 2013

    Naungana na mtoa maoni wa kwanza hapo juu. Hicho kiti amekiacha baada ya miaka miwili na zaidi, kwa nini wanamuaga sasa hivi. Sipati mantiki hata kidogo. Ilipaswa aagwe walau katika mkutano wa kwanza wa bunge mara baada ya kumwachia kiti Mama Anna. Very poor planning of events

    ReplyDelete
    Replies
    1. AnonymousJune 23, 2013

      Wewe ni makatibu wakuu wa wizara zote waliostaafu 4 years ago kuanzia hapo .Hapa mzazi karudi kutoka Dodoma na TV LED 66 inch na watapiga decoration nyumba nzima ( carpet na couches) na mzazi anafanya kazi consultant sehemu nyeti .

      Delete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...