Bw. Mustafa Haji Abdinur mwandishi kutoka Somalia anayeandikia AFP akizungumza  mbele ya Baraza Kuu la  Usalama la Umoja wa Mataifa, wakati Baraza hilo siku ya jumatano lilipojadili  usalama wa waandishi wa habari katika maeneo yenye migogoro,  Bw. Abdinur ambaye amejifundisha mwenyewe  uandishi  wa habari alieleza kwamba pale alipo ni kama maiti inayotembea na kwamba ni suala  la muda tu yeye kuuawa kutokana na ukweli kwamba waandishi wenzake wengi wamekwisha kuuawa nchini Somalia.  Hii ili kuwa ni mara ya kwanza kwa waandishi wa kimataifa kuzungumza ndani ya Baraza hilo
Bw. Richard Engel kutoka NBC News mmoja kati ya waandishi wanne walioalikwa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa  kueelezea uzoefu wao na  mikimikiki wanayokumbana nayo wanapotekeza majukumu yao ya kiuandishi.  Bw. Engel ambaye amesema amewahi kutekwa, alilitaka  Baraza Kuu la Usalama  linapojadilia kuhusu dhana nzima ya usalama wa waandishi, kujadili pia  ni nani hasa  mwandishi wa habari  anaye stahili ulinzi na akahoji kama  wanaharakati ambao nao wanachukua picha  za matukio mbalimbali na kuzipost kwenye mablog kama nao ni waandishi wa habari.  pembeni yake ni Bi. Kathleen Carroll,  ambaye ni mhariri mtendaji wa  Associated Press na Makamu mwenyekiti wa Bodi ya Kamati ya  Kulinda   Waandishi ( CPJ) yeye  katika mchango wake alisema licha ya kwamba waandishi wengi wanapoteza maisha  wakati wakitafuta habari kwenye maeneo yenye migogoro lakini waandishi watano kati ya sita wanauawa  ndani ya nchi zao wakati wakitimiza majukumu yao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...