Meneja wa shirika la Ndege la Emirates Tanzania Abdulaziz Al akizungumza na waandishi wa habari katika hafla ya Futari  iliyoandaliwa na shirika hilo kwa ajili ya wateja wake, wafanya biashara na wadau mbalimbali nchini. Hafla hiyoya futari ilifanyika katika Hoteli ya Hyatt Regency Dar es salaam
 Ofisa wa Emirates Bi Lubna (kati) akiwa na baadhi ya wadau waliofika katika futari hiyo
Meneja wa Emirates katika uwanja wa ndege wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam Ustaadh Aboubakar Jumaa (kulia) akiwa na wadau waalikwa katika futari hiyo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 12, 2013

    wewe sheikh issa michuzi wakati mwingine sio vibaya nawewe ukapiga kanzu sehemu kama hizo usijisahau sana wewe ni issa

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 13, 2013

    Asalam alaykum.
    Kwani ninani amesema kama kanzu ndio inayo mfanya mtu kuwa muislam?

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 13, 2013

    Alaykum Salaam!

    Naam Mdau wa Pili umenena, hii imekuwa ni tabia MBAYA SANA ya wengi wetu mfano unapo msalimia mtu ukiwa hujavaa Kofia ya ''Bargashia'' au Kanzu kwa kumpa 'Assalam Aykum' yeye inawezekana kabisa atanyamaza ama ataitikia kwa kejeli sana kama mojawapo ya hivi hapa chini.

    1.MSALIMIAJI:''Assalam Alaykum''
    MWITIKIAJI ''Salaaaaam'' !

    2.MSALIMIAJI: ''Assalam Alaykum''
    MWITIKIAJI ''Nini khabar'' !

    3.MSALIMIAJI: ''Assalam Alaykum''
    MWITIKIAJI ''Khaifa khabar'' !

    4.MSALIMIAJI: ''Assalam Alaykum''
    MWITIKIAJI ''Msalaaaam'' !

    5.MSALIMIAJI: ''Assalam Alaykum''
    MWITIKIAJI ''Vipi hali'' ?

    Jamani SALAMU ni MOJA YA IBADA KUBWA SANA KAMA ITAITIKIWA KWA NAMNA INAVYOSTAHILI.

    Hata Salamu inkuwa tabu?, inakuwa kama mtu ukiitikia sawasawa labda kama ulikuwa na LAKI MOJA mfukoni utakuta ELFU KUMI imepungua kwa kuitikia vyama salamu?

    Tunakwenda wapi?

    Ni muhimu tuchukue Mwezi huu Mtukufu wa Ramadhan kama Mafunzo ya kujirekebisha tabia hizi chafu kama KUWATATHIMINI WATU KWA MAVAZI

    Mfano Ankal amevaa vazi zuri tu la Kistaaarabu kuna tatizo gani hapo?

    Mfano unaposalimiwa ukiitikia vizuri kuna tatizo gani hapo?

    TUBADILIKE!



    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 13, 2013

    Namuunga Mkono Mdau wa 2 Mdau,

    Uislamu wa mtu hautathiminiwi kwa kuvaa Kanzu peke yake, Kuwa na ndevu nyingi,kuweka HINA kwenye madevu ama kuvaa Kibandiko peke yake,

    Imani ni Nafsi ya mtu, ungetoa dosari ya vazi kama vazi lingekuwa sio la stara.

    Lakini hiyo aliyovaa Abkali hapo inakubalika hata kuendeshea Ibada.

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 13, 2013

    Ankal yupo na Suti yake ya Kazini Serikalini Wajameni!

    Sasa mnafikiri kule Serikalini Ofisi Kuu wanavaa nguo zipi, naye inawezekana ametokea Ofisini moja kwa moja hadi kwenye Futari?

    Mnajuaje, labda pale nyumbani akina Selah walikuwa wanaandaa futari huku Kanzu ilikuwa ingali sandukuni na haijapigwa pasi?

    ReplyDelete
  6. AnonymousJuly 13, 2013

    Mdau wa Pili juu kazi tunayo na ndugu zetu pmoja na Mdau huyo wa Kwanza juu wanaojiona wao ndio Waisilamu safi zaidi kuliko wengine.

    Zaidi aniyetoa kasoro kwa kutovaliwa kwa vazi la Kanzu, pana wale Maulamaa wetu wanapo salimiwa ASSALAM AALYKUM!, wao hujibu kwa Staili ya Passport size ALAYKUM!

    Jamani, jamani, jamani, acheni mchezo ktk Dini ya Mwenyezi, hayo ya uitikiaji wa harau namna hiyo amefundisha Nabii gani?

    Hivi ndivyo Mtume alitufundisha uitikiaji wa salamu kwa nusu mkate kama hivyo?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...