Onyesho kubwa la kimataifa "International African Festival Tubingen 2013,linatalajiwa kuanza tarehe 8 hadi 11.Augost 2013,mjini Tübingen, jirani na Stuttgart huko Ujerumani. Maonyesho hayo ya aina yake yanatarajiwa kuhudhuriwa na watu zaidi ya 100,000 kutoka sehemu mbali mbali duniani.

wanasanii zaidi 600 zikiwemo bendi za muziki za kiafrika zitatumbuiza katika maonyesho hayo makubwa ya kiafrika barani ulaya.

Bidhaa na sanaa kutoka nchi mbali mbali za kiafrika ndizo zitakaonyeshwa katika maonyesho hayo,kutakuwa na mikutano katika ya wafanyibiashara wa kiafrika na wa Ujerumani kwa lengo la kukuza uhusiano wa kibiashara.

Onyesho hilo pia litaudhuriwa na mabalozi na wawakilishi wa nchi za kiafrika nchini Ujerumani,pamoja na viongozi wa jumuiya za kiafrika nchi ujerumani.

Maonyesho ya "International African Festival Tubingen " yanayo andaliwa na shirika lisilo la kiserekali Afrikaktiv e.V, chini ya mkurugenzi wake Madam Susan Enih Tatah,maonyesho hayo yanakuwa kwa kasi kubwa na kuwa na mvuto wa maelfu ya watazamaji.

Kwa wale wanao shiriki au kuhudhuria maonyesho hayo wanaweza kuwasiliana at Susan Enih Tatah – Founder & CEO
AFRIKAKTIV e.V
Call:+49(0)15210910374

kontakt@afrikafestival.net

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...