Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano Kimataifa, Balozi Rajabu Gamaha ambaye pia ni Mwenyekiti wa Mkutano wa Makatibu Wakuu wa Mambo ya Nje  wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) akifungua rasmi mkutano huo uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam tarehe 11 Julai, 2013. Mkutano huo ni maandalizi ya Mkutano wa Mawaziri utakaofanyika tarehe 13 Julai, 2013.
Balozi Gamaha (wa pili kutoka kushoto) akiwa na Kamishina wa Magereza wa Afrika Kusini, Bw. Tom Moyane (wa pili kutoka kulia), Mkurugenzi Mkuu wa masuala ya Usalama wa Namibia, Bw. Ben Likando (Kulia) na Mkurugenzi wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya SADC, Luteni Kanali Mstaafu, Tanki Mothae (kushoto) kabla ya ufunguzi wa mkutano huo.
Wajumbe wa Tanzania wakimsikiliza Balozi Gamaha (hayupo pichani) wakati wa ufunguzi wa mkutano huo. Kulia ni Mhe. Radhia Msuya, Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini na Balozi Naimi Aziz, Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
Wajumbe kutoka nchi wanachama wa SADC wakimsikiliza Balozi Gamaha (hayupo pichani) wakati wa ufunguzi wa mkutano huo wa Makatibu Wakuu.
Wajumbe wengine wakati wa ufunguzi.
Wajumbe wa Sekretarieti ya SADC.
Picha na Reginald Philip na Olga Chitanda    

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...