Kikosi cha Timu ya Taifa (Taifa Stars) kikiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Entebe nchini Uganda jioni ya leo,tayari kwa mtanange wa marudiano na timu ya Taifa ya nchi hiyo utakaopigwa mwishoni mwa wiki hii.
 Kikosi cha Taifa Stars kikiwa uwanja wa ndege wa Mwanza kikisubiri usafiri kilikutana na Rais Jakaya Mrisho Kikwete ambaye naye alitua hapo kwa muda akielekea Bukoba kwa ziara ya siku sita mkoani Kagera
 Rais Kikwete akisalimiana na wachezaji wa Taifa Stars jijini Mwanza
 Rais Kikwete akiwatakia Taifa Stars kila la heri katika mchezo wao wa marudiano

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 25, 2013

    hivi jamani mbona baadhi ya watu sio wastaarabu au niseme ndio UJINGA wa simu kweli unasalimiana na rais kiongozi wa nchi uko na kijisimu cha mchina mkononi

    kweli hii heshima yaani hata baba yako kumpa mkono na simu mkononi ni dharau kubwa au mtu yeyote yule unaemuheshimu nashangaa sana sisi watanzania tuliowengi sana tunaulimbukeni sana wa simu

    utamkuta mtu anafanya kitu cha maana sana ila simu iko mkononi jamani simu kweli niyamkononi ila sio wakati wote tubadilikeni jamani watanzania

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 25, 2013

    Naungana na Mdau wa Kwanza:

    Simu Mikononi ni tabia ya Ubwege sana!!!

    Simu kitu gani?

    Jambo lingine pana ile tabia ya mtu muda wooote yupo buzy na simu yake, unakuta anapekua ktk fone book na kupiga simu bila umuhimu wowote au anatumia muda mwingi ku-chat bila mpango wowote.

    Tanzania ni muhimu tukabadilika kwa kuacha hulka za ajabu ajabu, hubu tazameni unafiukia kipindi unasalimiana na Raisi wa nchi yako lakini simu bado ipo mkononi!!!

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 25, 2013

    Taifa Stars ni wakati wenu sasa kilpa Fadhila!!!

    Raisi Jakaya Mrisho Kikwete ameshawabeba saana kwa Ufadhili wa Michezo lakini bado hambebeki, jamani hii sasa ni aibu.

    Hebu tumieni Mechi hii angalau mumfanye JK afarijike kidogo angalau kwa hasara kubwa alizotumi kwenu lakini hatusongi mbele kila uchao.

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 25, 2013

    Nakubaliana na mdau Stars wajitume katika mechi hii ya pili na Cranes-uganda washinde mchezo huu muhimu saana,wakifungwa tena basi kama nilivyosema mwanzoni kufanyike mabadiliko kuanzia kocha na wachezaji mapema,tunataka kuwaona wachezaji wanaocheza kwa maelewano ya ushindi katika mechi za kimataifa hatuwataki wachezaji wa majaribio kufuatana na majina au klabu wanazocheza katika ligi.
    mikidadi-denmark

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...