Sekoutoure Khalifa Mndeme (24 Julai 1965 – 10 Julai, 2011)

Tarehe 10 Julai, 2011 Sekoutoure ‘Toure’ Khalifa mzawa wa Usangi, Wilaya ya Mwanga, mkazi wa Kunduchi-Mtongani, Dar es Salaam, aliaga dunia katika Hospitali ya Apollo, nchini India.

Jamii ilitoa msaada mkubwa tangu pale Toure alipolazwa Hospitali ya Aga Khan mwishoni mwa Juni, baadaye akahamishiwa Taasisi ya MOI (Muhimbili) na kisha kupelekwa India kwa uchunguzi zaidi na matibabu, hadi alipofariki. Tuliendelea kupata ushirikiano wenu hadi mwili wa Toure ukarejeshwa Dar toka India tarehe 13 Julai na hatimaye kusafirishwa kwenda Usangi–Ngujini kwa mazishi, Ijumaa, trh 15 Julai, 2011.

Familia ya Sultani na Omari Muyanza ya Usangi Mwanga, ya Hemedi Mwamtemi ya Lushoto na ile ya Toure (mjane Halima H. Mwamtemi, wanawe Khalifa (18), Hemedi (15) na Bi Hafsa “Doctor” (8) walifarijika mno kwa upendo na ushirikiano wa ninyi ndugu, jamaa, majirani na marafiki.

Leo tarehe 10.07.2013, Bw. Sekoutoure ‘Toure’ Khalifa ametimiza miaka miwili (2) tangu alipofariki.

Familia inafarijika sana kwa upendo na ushirikiano unaoonyeshwa na ndugu, jamaa na marafiki tangu mpendwa wetu alipotutoka hadi leo. Tunawashukuru sana na tunawaomba muendelee na upendo mlionao kwetu. Pia, tunawaomba muendelee kumuombea ndugu yetu kwa Allah.

Toure; ni kweli kwamba umetutoka kimwili, lakini utabaki ndani ya mioyo yetu daima. Upendo, ucheshi, hekima na busara zako zitabaki kama dira na changamoto ya kuwania ubora kwa sote ulotuacha nyuma.
“INNA LILLAH wa Ina ILLAYH RAJ’UNN – Kwa Mola tumetoka na Kwake tutarejea.” - Al Quran, Sura 6:128

MOLA AILAZE ROHO YA SEKOUTOURE MAHALI PEMA PEPONI - AMINA.



Shukran

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. RIP Sekoutore, nilifanya kazi na huyu mpendwa CRDB LUmumba miaka ya 1993 hadi 94.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...