Karibu katika mahojiano baina ya Jamii Production na waTanzania wanaomiliki Chuo cha Uuguzi cha Kansas Ndg Michael Katunzi na Ndg Robert Otto. Katika mahojiano haya, wanaeleza mambo mbalimbali ikiwemo walipopata na walivyopata wazo la kuanzisha chuo hiki, walivyoanzisha na walipo hivi sasa, changamoto walizokutana nazo kuanzia kuanzisha mpaka kilipo sasa, mafanikio yao na ya chuo chao pamoja na mipango yao juu ya chuo hicho kilicho katika nafasi za juu miongoni mwa vyuo vya uuguzi jimboni humo. Karibu uungane nasi

Wanafunzi wa Chuo cha Uuguzi cha  Kansas College of Nursing wakiwa darasani 

Wafanyakazi wa Kansas College of Nursing 

Wanafunzi wa Kansas College of Nursing

Wanafunzi wa Kansas College of Nursing
Mahojiano baina ya Jamii Production na waTanzania wanaomiliki Chuo cha Uuguzi cha Kansas Ndg Michael Katunzi na Ndg Robert Otto


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 30, 2013

    Hongera wadau wa "Care homes US" kwa mafanikio. Miaka ya tisini mpaka elfu mbili kulifumka vyuo vya "Computing" huku Ughaibuni. Sasa vyuo hivi vingi vimefungwa kwa kukosa wanafunzi. Ushauri wa bure msijisahau na mafanikio mliyopata hivi sasa. Siri ya mafanikio ya nyanja ya elimu ni upatikanaji wa kazi.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 30, 2013

    Hongereni sana je wanatoa course za level gani? naweza kupata maelezo ya kupata nafasi?

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 30, 2013

    Hongereni sana. Wadau naomba kuuliza nataka kwenda kusoma chuo cha unesi USA je ni dollar ngapi kwa mwaka. Msiponde oooh mbona unaenda kusomea unesi sababu najua nifanyalo, mwenye jibu anisaidie tu.
    Asanteni

    ReplyDelete
  4. Ankal

    Kwa kweli, hao waBongo wawili wamenifurahisha sana. Nilisikiliza hayo mahojiano yao, nikaishiwa nguvu kwa jinsi walivyo makini katika kujiwekea malengo na kuyafuatilia. Halafu wanajiamini kabisa, na uwezo wanao. Ni mfano wa kuigwa.

    Nawaombea mafanikio zaidi na zaidi. Huwezi kujua, kesho na keshokutwa wanaweza wakafungua chuo au vyuo Tanzania, wakaineemesha nchi kwa uzoefu na elimu waliyo nao.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...