Na A bdulaziz Video Lindi

Wakazi wa Manispaa ya Lindi, kwa takribani juma moja sasa, wanakabiliwa na ukosefu mkubwa wa upatikanaji maji safi na salama na kulazimika kutumia maji ya visima vya kienyeji vilivyochimbwa kwenye baadhi ya makazi ya watu.

Baadhi ya wananchi waliohojiwa na Mtandao huu kuhusiana na tatizo hilo, wameonesha hofu yao ya kutokea kwa milipuko ya magonjwa ya matumbo ikiwemo kipindupindu kwa vile maji ya visima wanayotumia kwa sasa siyo safi na salama kwa matumizi ya binadamu.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa Maji safi na Usafi wa Mazingira Lindi mjini(LUWASA), Idrisa Sengulo, pamoja na kukiri kuwepo kwa tatizo hilo kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wa Mamlaka, amewaomba radhi wananchi kwa tatizo hilo ambalo amesema kama mambo yakienda vizuri linaweza kutatuliwa ktk kipindi cha siku mbili zijazo.

Amesema mahitaji ya maji kwa wakazi wa Manispaa ya Lindi ni lita milioni 5 kwa siku, ikilinganishwa na lita lita milioni 1,340,000 tu kwa siku zinazopatikana kwa sasa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 27, 2013

    Nadhani maji ni tatizo kubwa ambalo limefumbiwa macho na kubezwa na viongozi kwa kipindi cha tangu uhuru, juhudi za kuliondoa hili tatizo hazi akisi ukubwa wa tatizo licha ya utajiri wa vyanzo vya maji tulinao.Ifike wakati sasa tatizo la maji nalo lipewe kipaumbere kama malaria au kama tatizo la rushwa(japo ni propaganda).Maji ni uhai,maji ni afya, ebu jaribu kuangalia kiasi cha upatikanaji wa maji na matumizi yake kwa siku ktk taarifa hii ya huko lindi ndipo utakapo ona kwamba wengine wanakunywa tope au hata maji ya bahari ila hawasikiki kabisa.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...