Mshauri Mkuu wa Kampuni ya Mabibo Beer,Wine & Spirits Tanzania,James Rugemarila (kulia) akisisitiza jambo wakati akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya Wajibu wa Kutii amri ya Mahakama ya Kinondoni jijini Dar es Salaam,baada ya kutokea uuzwazi wa Bia za Windhoek kinyume na taratibu kwa katika Hoteli ya Land Mark wakati bado Mahakama inaendelea kufanya kazi yake.hali hiyo imekuja baada ya kubainika kuwa unauza Bia za Windhoek ambazo ni za magengo.Kampuni ya Mabibo Beer,Wine & Spirits Tanzania ndio imepewa kibali na uhalali wa usambazaji wa Bia za Windhoek hapa nchini,zinazotengenezwa na Kampuni ya Namibia Breweries.Kushoto ni Meneja Mkuu wa Mabibo Beer,Wine & Spirits Tanzania,Neil Stainton akifafanua jambo mbele ya Waandishi wa Habari (hawapo pichani) wakati wakitoa taarifa ya uhalali wa usambazaji wa Bia za Windhoek zinazotengenezwa na Kampuni ya Namibia Breweries,leo kwenye Ukumbi wa Elkad 24,Mikocheni jijini Dar.
 Meneja Mkuu wa Mabibo Beer,Wine & Spirits Tanzania,Neil Stainton akifafanua jambo mbele ya Waandishi wa Habari (hawapo pichani) wakati wakitoa taarifa ya uhalali wa usambazaji wa Bia za Windhoek zinazotengenezwa na Kampuni ya Namibia Breweries,leo kwenye Ukumbi wa East 24,Mikocheni jijini Dar.
Mkurugenzi Mtendaji wa Mabibo Beer,Wine & Spirits Tanzania,Benedictor Rugemarila (kulia) akisisitiza jambo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 11, 2013

    Inakkuwaje hii kampuni ipewe umiliki wa usambaji peke yake???soko huru la biashara liko wapi???mie sikubaliani nao hawa jamaa..biashara ni ushindani sio waachiwe wao tu hii ni karne 21!!

    ReplyDelete
    Replies
    1. AnonymousJuly 12, 2013

      Wewe ni hujui unaloongelea, wao ndio wanakibali kama sole suppliers nchini Tanzania hii kitu ipo duniani.

      Wao ndio wamekuwa wa kwanza kuleta bia hizo, sasa wanauza kwa bei ya kiwandani then ndio watu wananunua na kuuza kwa wateja.

      Kuwa sole supplier basi hiyo hoteli ingeanza wao kupata bia hizo kabla ya hawa kuzileta na kuzitangaza nchini. Do you get that?

      So wanaibia kwenda kuleta bia toka nje ya nchi bila kupitia kwa sole supplier.

      Hapa niameandika ili ujifunze kama let's say kesho unapewa tender ya kufanya kitu hata tokea hapo bongo, unaambiwa ni wewe tu ndio utasambaza. Wateja wanaambiwa ni wewe etc

      Kesho yake unakuta mtu mwingine anafanya kama wewe kweli utanyamaza? Na hapo umesha invest pesa kibao zako unasubiri faida irudi?

      Acheni wivu wa kudandia kazi za watu na kusubiria mwishoni kuiba nyie haya mahakama itasema.

      Delete
  2. AnonymousJuly 12, 2013

    Inafurahisa kuona mke na mme wakishirikiana ki biashara. Si kawaida.Familia zingine, mke hajui mme ana nini na mme hajui mke ana nini. Mwisho wa siku mme akiondoka duniani anaondoka ki vyake na mke kadhalika. Nawashauri wenye maisha ya namna hii wabadirike vinginevyo wanadnaganyana

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 12, 2013

    Anony wa pili msamehe huyo anony wa kwanza maana hajui dunia ya biashera inavyokwenda. Yeye akikopi rekodi ya mtu ya mziki anadhani ni sawa tu. Dunia ya biashara haiko hivyo. Mikataba lazima ihashimiwe. Ujanja ujanja haufai.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...