Adam Sykes,Mrs Mganda,Ashura.

Na Swahili TV Washington DC
Omar Sykes mwanafunzi  raia wa Tanzania aliyeuwawa  katika jiji la Washington, huenda akaenziwa kwa mtaa mmoja kupewa jina lake ili kuweka kumbukumbu na ujumbe kwa wote walioathirika na  mauaji ya bunduki mitaani jijini Washington, Dc,  na Marekani kwa ujumla. Kama pendekezo hilo litapitishwa atakuwa mtanzania wa kwanza kupewa mtaa nchini Marekani.

Akiongea katika shughuli ya kuuaga mwili wa marehemu Omar Sykes, meya wa  jiji la Washington, mstahiki Vicent Gray,  alisema kuwa anatarajia kupendekeza katika kikao kijacho cha halimashauri ya jiji mwezi Septemba  kubadilisha mtaa wa Fairmont  St, ambako mauti yalimkuta  ili uitwe Omar Sykes Street.
Meya Gray aliongeza  kusema kuwa  kitendo hicho kitakuwa ni ujumbe kwa nchi nzima ya Marekani  katika kuelezea ubaya wa ghasia za mauaji ya risasi mitaani. Marehemu Omar aliuwawa kwa risasi akiwa katika mazingira ya karibu na chuo kikuu anachosoma cha Howard.
Katika shughuli  hiyo ya kuuaga mwiili , Swahili TV ilifanikiwa kuona baadhi ya viongozi maarufu waliohudhuria  shughuli  hiyo kama Naibu waziri wa mambo ya nje wa Marekani anayeshughulikia masuala ya Afrika Bi Jendayi Frazier alikuwa naibu waziri wakati wa utawala wa Bush 2005-2009.
Akiongea na Swahili TV, baba wa marehemu bwana Adam Sykes  ambaye naye alikuwepo katika shughuli hiyo, alisema ni heshima ya pekee kwa taifa kubwa kama hili kumuenzi  mwanae kwa kumpa jina la mtaa.

“Ni heshima ya aina gani kwa  taifa  kubwa kama hili kumuenzi  mwanangu  kwa kumpa mtaa”Alisema kwa majonzi huku akionesha furaha ya kupata heshima hiyo, bwana Sykes ambaye yeye na kaka Allyas Sykes waliwasili jumanne wiki hii nchini Marekani.
Swahili TV iliongea na  wananchi mbalimbali waliohudhuria  shughuli hiyo ambao  wengi walionyesha  hali ya majonzi   ya kifo cha kijana huyo,  mahojiano  ya Swahili TV na  baadhi ya viongozi wa serikali na Uongozi wa shule yatachapishwa na kuonyeshwa  blog yetu.www.swahilitv.blogspot.com

Kwa picha za event ya Celebrating the life of Omar Sykes
BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 7 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 12, 2013

    MUNGU AMLAZE PEMA PEPONI NI HURUMA ..
    ILA SIJAELEWA INAONEKANA WENGI WAMEFURAHIA MTAA KUPEWA JINA BADALA YA KUANDAMANA MAUAJI YANAYOTOKEA U.S.A
    UKITAZAMA MAUAJI KAMA HAYA SI MARA YA KWANZA KUTOKEA UKIACHILIA YA RAIA WENYEWE SIE TULIOPO MJE TUNAANGALIA TV CHANEL TLC NDO UTAONA HUKO KULIVYO

    HATA WAWEKE JINA MAUAJI YA KAMA HAYO NI VIGUMU KUISHA WATU WANAMILIKI BUNDUKI ,VISASI NK

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 12, 2013

    Pole sana mzee Sykes, mama, ndugu, jamaa na marafiki wote. Binafsi nadhani ni jambo jema kama utafanyika utaratibu wa kutafuta haki(justice). Kwa kuwa tunasikia nchi hiyo ni nchi ya haki, siyo? Ingawa tutakubaliana kuwa safari ya kudai haki ya kuuwawa kwa mtoto wako itakuwa ngumu na ndefu, lakini hatimae inaweza kupatikana. Ila inabidi serikali yetu iwe kama serikari za nchi zingine, yaani ikusaidie/ijisaidie! Na haki ikifanyika ni vema kwa upande wako kama mzazi na pia ni kinga kwa watu wengine walioko huko.

    Jina la mtaa waache waite, hata wakitaka kuita mji ni sawa tu. Maana jina ni jina, baada ya miaka kadhaa pia litaondolewa na kuwekwa jina jingine. Sisi tunacholilia ni haki, haki ndiyo itakayotulinda kwa kutuletea AMANI. Amani itatupa maisha marefu.

    Watu wengi huamua kudai haki kwa kuwa ni jambo zuri au jema. Achilia mbali matokeo yake: Mtu apatapo haki yaku hufurahi, na hata kama haikupatikana bado kuna sehemu ya furaha kwa sababu alijaribu/ ulijaribu kudai.Kama haki isipopatikana basi fimbo ya myonge hulipwa na Mwenyezi Mungu

    Kwa vipi mpaka sasa hatujaambiwa ni nini hasa, je alikuwa na maadui au ni bahati mbaya au ni vipi hasa!?
    Fikilia kama ingekuwa ni mtu wao amefanyiwa hivyo hapa kwetu. Yamkini nchi nzima sasa hivi wote tungekuwa tunaruka kichura chura, toka Mkulu mpaka Chinga.
    Namaliza kwa kusema tena pole na Mungu amlaze Marehemu mahala pema peponi- Amina

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 12, 2013

    Poleni sana wafiwa wote, zaidi na zaidi mwazazi wa marehemu Omar Sykes. Allah awape subira kubwa sana na kumuombea dua mtoto wenu kwa huko aendako kwa muumba apate jazaa njema na kuwa miongoni mwa waja wema amin.

    Kumbukumbu ya maremu Omar Sykes ni jambo zuri ila isiifanye familia kukosa haki yake juu ya mtoto wenu. kazeni kamba kwa kudai haki itendeke mpaka mwisho wenu na Allah atasidia in sha allah.

    Wote tunafahamu machungu ya kuondokewa ni makubwa sana kwenu kwani nyota mlioitegemea kuangaza baadae imezimika hafla kung'aa, lakini Allah ndie mjuzi wa yote na kila kitu.

    Inah lilah waina ilayhi rajium.

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 12, 2013

    Ujumbe mzuri kabisa.

    Poleni wafiwa

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 12, 2013

    Poleni wafiwa. Pia jaribuni kutafuta mwanasheria atakaye fungua kesi ya kulipwa gharama za kuuwawa mtoto wenu. Hizi nchi za ughaibuni kama wangalijua kuruga basi ingekuwa hatari kuliko Afrika maana choyo na visasi ni vingi.

    ReplyDelete
  6. AnonymousJuly 12, 2013

    Inna Lillah wa Inna Ilayhyi Rajiuuun!

    ReplyDelete
  7. To ADAM, "Inna Lillah wa Inna Illahi Rajeoon," Adam pole sana sana, I know what you are going thru, because I also went thru of what you are, so I know how it feels, Inshaalah ALLAH atakupa SUBRA that is not a punishment but a trial, inshaalah utashinda To MDAU No.One "Ada ya mja kunena Muungwana ni Vitendo," shika bango uanze kuandamana kina sie tutajump into the wagon, It is easier say than done, Omar rest in peace justice will be done Inshaalah, without MAANDAMANO.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...