Afisa wa bodi ya michezo ya kubahatisha nchini,Bw.Bakari Maggid akiweka karatasi zenye majina ya washiriki wa Promosheni ya lipa kwa M pesa na Ushinde ukiwa Sabasaba na kujishindia zawadi ya shilingi Elfu 40 sanjari na muda wa maongezi wa shilingi 1000 kila siku ambapo washindi watano walipatikana,Promosheni hiyo inaendeshwa na Vodacom Tanzania wengine wanaoshuhudia toka kushoto ni Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania Matina Nkurlu.
Mkazi wa jijini Dares Salaam Bi.Khadija Abdallah (kushoto) akishuhudiwa na Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania Bw. Matina Nkurlu wapili toka kushoto na Afisa wa bodi ya michezo ya kubahatisha nchini,Bw.Bakari Maggid akichukua karata yenye jina la mshindi wa kwanza kati ya washindi watano waliojishindia shilingili elfu 40 sanjari na muda wa maongezi wa shilingi 1000 kila mmoja katika promosheni ya fanya malipo kwa huduma ya M PESA ukiwa Sabasaba.
Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania Bw.Matina Nkurlu akiongea kwenye simu na mmoja kati ya washindi watano waliojishindia shilingi elfu 40 kila mmoja kwenye droo ya lipa kwa M pesa na Ushinde ukiwa Sabasaba sanjari na muda wa maongezi wa shilingi 1000 kila siku.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...