Mmoja wa vijana wanaojishughulisha na kilimo cha mboga mboga katika Bonde la Mlowa katika Halmashauri ya Mji wa Makambako Mkoani Njombe, Saimon Mdee (kushoto) akimsikiliza kwa makini Mkurugenzi wa Mamlaka ya Uendelezaji wa Bonde la Mto Rufiji (Rubada), Bw. Aloyce Masanja alipowatembelea vijana hao katika shamba la maparachichi na mbogamboga, ikiwa ni katika kuhamasisha kilimo kupitia Mpango wa Ukuaji wa Kilimo katika Ukanda wa Kusini mwa Tanzania (SAGCOT).
Mkulima wa mboga mboga katika Bonde la Mlowa katika Halmashauri ya mji Makambako Mkoani Njombe, Bw. Joseph Chengula (Kulia) akimwonyesha ukubwa wa bonde la Mlowa, Mkurugenzi wa Mamlaka ya Uendelezaji wa Bonde la Mto Rufiji (RUBADA) Bw. Aloyce Masanja( katikati)  alipofanya ziara ya kutembelea kambi za vijana wanaojishughulisha na kilimo katika mji huo jana.  Mkurugenzi huyo alikua katika ziara ya kuhamasisha kilimo kupitia Mpango wa Ukuaji wa Kilimo katika Ukanda wa Kusini mwa Tanzania (SAGCOT).  Kulia ni mkulima mwingine wa mbogamboga, Bw. Silas Martin.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...