Mmoja wa vijana
wanaojishughulisha na kilimo cha mboga mboga katika Bonde la Mlowa katika Halmashauri
ya Mji wa Makambako Mkoani Njombe, Saimon Mdee (kushoto) akimsikiliza kwa
makini Mkurugenzi wa Mamlaka ya Uendelezaji wa Bonde la Mto Rufiji (Rubada),
Bw. Aloyce Masanja alipowatembelea vijana hao katika shamba la maparachichi na
mbogamboga, ikiwa ni katika kuhamasisha kilimo kupitia Mpango wa Ukuaji wa
Kilimo katika Ukanda wa Kusini mwa Tanzania (SAGCOT).
Mkulima wa mboga
mboga katika Bonde la Mlowa katika Halmashauri ya mji Makambako Mkoani Njombe,
Bw. Joseph Chengula (Kulia) akimwonyesha ukubwa wa bonde la Mlowa, Mkurugenzi
wa Mamlaka ya Uendelezaji wa Bonde la Mto Rufiji (RUBADA) Bw. Aloyce Masanja(
katikati) alipofanya ziara ya kutembelea
kambi za vijana wanaojishughulisha na kilimo katika mji huo jana. Mkurugenzi huyo alikua katika ziara ya kuhamasisha
kilimo kupitia Mpango wa Ukuaji wa Kilimo katika Ukanda wa Kusini mwa Tanzania
(SAGCOT). Kulia ni mkulima mwingine wa
mbogamboga, Bw. Silas Martin.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...