Ankal akiwa katika sebule ya nyumba aliyokuwa akiishi Mzee Nelson Mandela Mtaa wa Vilakazi namba 8115 huko Orlando ya Magharibi, Soweto, Afrika Kusini. Hii ilikuwa Julai 18, 2010 wakati wa kuadhimisha Hepi Besdei ya miaka 92 ya kuzaliwa kwa Madiba. Leo Globu ya Jamii inaungana na wadau wote duniani kuadhimisha miaka 95 ya shujaa huyu wa Afrika anayependwa na kila mtu.
Ikumbukwe pia kwamba leo ni siku ya Kimataifa ya Mandela kama ilivyotangazwa na Umoja wa Mataifa mwaka 2011.
Tunamtakia aendelee kupata nafuu na aweze kuinuka kitandani huko hospitali alikolazwa kwa mwezi mmoja sasa ili apulize mishumaa yake na kukata keki huku sisi tukimwimbia HAPPY BIRTHDA MADIBA!!!!

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 18, 2013

    Yafaa sote tujiulize iwapo kuna kitu jamii itatukumbuka kwacho hapo uzeeni. Ona kila mtu anampenda na kumwona Madiba kama Babu yake. Tutende mema jamani.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 18, 2013

    Happy Birthday Baba Mandela! Nakutakia maisha marefu mengine na M/Mungu akupe ahueni ya haraka katika maradhi yako.

    Katika siku ya leo ni MANDELA DAY, na pia nashukuru kuwa leo ni siku yangu pia ya KUZALIWA!

    Najivunia sana tarehe na mwezi wa kuzaliwa kwangu kuwa sawa na wewe Mheshimiwa Mkuu wa Dunia.

    "HAPPY BIRTHDAY TO US"=Nelson Mandela + Peters Mhoja!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...