Waziri wa Ujenzi Dr.John Magufuli (kushoto) akisikiliza maelezo ya ujenzi wa barabara kutoka Ndundu-Somanga (km 60) mkoani Pwani jana kutoka kwa Mhandisi Mkazi kutoka kampuni ya ESG (Mouchel Parkman )alipotembelea kuangalia maendeleo ya ujenzi huo ambapo hadi sasa wameshalipwa kiasi cha shilingi 59 bilioni.
Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli(mwenye pama katikati) akitoa maagizo kwa meneja wa mradi wa ujenzi pamoja na Mhandisi mkazi wa mradi huo hawapo pichani jana alipotembelea mradi huo jana,ambapo Waziri Magufuli mna mwenedo wa kususua wa ujenzi huo. (kushoto) Ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Balozi Herbet Mrango.(kulia) Mkuu wa Mkoa wa Dsm Mecky Sadick.Picha na Mwanakombo Jumaa.
Baadhi ya shughuli za ujenzi mbalimbali za barabara zikiendelea.
.Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli (kulia) akiongea na baadhi ya wanakijiji wa Malendego jana wakati wa ziara yake ya kukagua ujenzi wa mradi ya barabara ya Ndundu- Somanga(km 60).
Baadhi ya wakazi wa kijiji cha Malendego mkoani Pwani wakimsikiliza Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli (hayupo pichani) wakati wa ziara ya kikazi
KAZI IPO; KM 60 HAZIJAISHA???
ReplyDeleteKM 60 NI HIFADHI YA TAIFA 2015.
ReplyDeleteShillingi billion 59 kwa kazi ya kilomita 60 ambazo hazijamalizika.
ReplyDeleteKwa mahesabu ya haraka kwa spidi ya kutoa takwimu kama Mh.John Pombe Magufuli ni kuwa kila kilmita moja gharama yake ni shilling Billioni moja ( Tshs. 59 Billioni / 60km.
Je, barabara ikijengwa kwa kutumia zege la simenti ambayo kila kitu kinapatikana Tanzania ujenzi wa barabara za zenge hauwezi kuwa nafuu?
Mdau
Ma- 'data'
Hivi kweli hakuna namna yakupunguza gharama za ujenzi wa barabara zetu? Hili nalo linabidi kujadiliwa kwa kina. Kila km 1 ni bilioni moja kweli?
ReplyDelete