Ujumbe wa viongozi kutoka wilaya ya Hai wakiwa na mwnyeji wao ambaye ni mratibu wa miradi mbalimbali ya maendeleo na pia ni diwani,Stina Johansson (wa tatu kulia).Wengine kutoka kulia ni Novatus Makunga[mkuu wa wilaya ya Hai],Clement Kwayu[mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Hai]Melkizedeck Humbe[Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Hai] na Ester Mbatiani ambaye ni Afisa mipango mkuu wa halmashauri ya wilaya ya Hai.

Na Richard Mwangulube

Halmashauri ya wilaya ya Hai,imeingia mkataba wa miaka minne wa ushirikiano na Manispaa ya Arvidsjaur nchini Sweden unaolenga katika maeneo ya kiuchumi na kijamii ukiwemo wa teknolojia ya kisasa ya udhibiti wa takataka kiuchumi kwa kuziwezesha kutengezwa upya bidhaa kwa ajili ya matumizi.

Mkataba huo ulitiwa saini wakati wa ziara ya ujumbe wa viongozi wa wilaya ya Hai uliyoongozwa na Mkuu wa Wilaya Hiyo, Novatus Makunga hivi karibuni katika makao Makuu ya Manispaa hiyo nchini Sweden.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...