Wafanyakazi wa Airtel wanategemea  kuiingiza rasmi promosheni ya Airtel money, Hakatwi mtu hapa kwenye mitaa mbalimbali ya jiji la Dar es salaam kuanzia jumatano wiki hii.
wafanyakazi wa kampuni ya mitandao ya simu za mkononi Airtel wanafanya hivyo kwa dhumuni la kuelimisha na kuikaribisha rasmi promosheni ya Airtel money, Hakatwi mtu hapa kwa watanzania.
Airtel imechukua maamuzi hayo katika muendelezo wa kuhakikisha inajenga mahusiano mazuri kati ya wafanyakazi wa kampuni hiyo na wateja wake na kuwapatia huduma bora kwa kuwatembelea maeneo walipo.
Akizungumza juu ya ziara hiyo, Meneja Uhusiano wa Airtel, Bw Jackson Mmbando alisema dhumuni la ziara hiyo ni kuhamasisha na kuwaelewesha wateja mbalimbali wa Airtel juu ya huduma mbalimbali ambazo zimekuwa zikitolewa na kampuni hiyo ya mitandao ya simu za mkononi hususani promosheni mpya ya Airtel money, hakatwi mtu hapa.
“Tumeamua kuingia mtaani kuwahamasisha wateja wetu juu ya huduma ya Airtel Money Yatosha kwamba inamuwezesha mteja yeyote wa Airtel kutuma na kupokea pesa bure katika Mtandao wowote hapa Tanzania,” alisema Mmbando.
Kwa mwaka huu ziara hii inakuwa ni ziara ya tatu kufanywa na kampuni hiyo ya simu za mkononi baada ya ziara nyingine mbili zilizofanywa hapo awali mwaka huu kuwa na mafanikio makubwa sana kwa kuweza kupata nafasi ya kuweza kukutana na wateja wao kwa kutoa Elimu  na kuweza kuwasaidia katika  maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...