Na Abdulaziz video,kilwa
Mbunge wa jimbo la Kilwa kusini Saidi Bungara (CUF) amelaani kitendo
cha baadhi ya wananchi mikoa ya Lindi na Mtwara kwa kukwamisha juhudi za
serikali katika kuwaletea maendeleo wananchi kupitia uwekezaji wa gas
ya asili nchini
Haya ameyaeleza kwenye hafla fupi ya kutiliana sahini mkataba wa
ujenzi wa zahanati ya kijiji cha Nangurukuru kati ya halmashauri ya
wilaya Kilwa na kampuni ya Afrikan Energy Inayojihusisha na utafiti
wa mafuta na gesi.
Bungara alisema kitendo cha mwekezaji huyo kuwafanyia maendeleo
wananchi wa wilaya hiyo ni ishara tosha ya kutambua michango na
juhudi za wawekezaji katika kutoa huduma za kijamii kwa wananchi.
‘Kitendo cha mwekezaji wa pan African Energy kutoa misaada yenye
lengo la kuboresha huduma za kijamii zimethihirisha ukweli wa
serikali kuhusu faida na maana ya wawekezaji, sisiwa Kilwa hatuwaungi
mkono wa Mtwara tuna sema itoke tu” alisema Mbunge Bungara.
Alisema watu wa kilwa hawana sababu kupinga ya kupinga uwekezaji wa
namna yoyote kwani wanachohitaji ni maendeleo na sio vurugu na fujo
kama wanavyofanya wananchi wa mkoa wa mtwara kupinga kuondoka kwa
kesi .
Kwa upande wake Meneja wa huduma za jamii wa kampuni ya Pan Afrikani
Energy Andrew Kashangaki alisema kampuni inafadhili ujenzi wa
zahanati ya Nangurukuru na unatarajia kutumia zaidi ya shs milioni
234,714,980.
Kashangaki alisema sambamba na kusaidia ujenzi wa zahanati hiyo pia
kampuni hiyo inalipa ushuru wa huduma ambapo hadi sasa imelipa kwa
halmashauri hiyo zaidi ya shs milioni 638 na inatoa misaada mingine
katika sekta ya elimu.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...