Mkurugenzi Mtendaji wa umoja wa vilabu vya waandishi wa habari Tanzania (UTPC), Abubakar Karsan 

Na  Francis Godwin
HUKU kukiwa na taarifa ya  baadhi ya  wanahabari  mkoa  wa Morogoro ambao wanadai  kushindwa katika uchaguzi wa klabu yao kuanza mchakato wa kuanzisha klabu yao mpya  ,uongozi wa umoja  wa  vilabu vya  waandishi wa habari Tanzania (UTPC) umetoa onyo kali kwa  klabu ya moja morogoro Press klabu  kuwa kamwe klabu  hiyo hakitatambuliwa na UTPC itakuwa ni klabu ya  wanahabari wa  vijiweni.
Tamko  hilo limetolea  mjini Dodoma  leo na  Mkurugenzi Mtendaji wa umoja wa vilabu vya waandishi wa habari Tanzania (UTPC), Abubakar Karsan wakati wa mkutano mkuu maalum wa  kupitia rasmu ya katiba  mpya ya UTPC .
Bw  Karsan alisema  kuwa amepokea  taarifa  kutoka mkoa wa Morogoro kuwa kuna baadhi ya  viongozi wa  klabu  hiyo ambao  walishindwa kwenye uchaguzi uliowatoa madakani.
" UTPC inatoa onyo kali kwa  wanahabari  wanaoanzisha  klabu  hiyo ya moja morogoro Press Klabu kwani  hadi  sasa  kwa katiba ya UTPC kila mkoa  unapaswa  kuwa na klabu moja pekee na kwa mkoa wa Morogoro tunatambua klabu ya Moro Press klab pekee  si nyingine ....hatuwazuii kuendelea na mchakato  ila  sema  hiyo klab yao itakuwa ya  kijiweni haitatambulika kamwe na UTPC"
Bw Karsan  alisema  kuwa  wapo baadhi ya  wanahabari  wanaondolewa katika vyama vyao vya msingi kwa kwa utovu wa nidham na kukimbilia  kuanzisha klabu za uchochoroni ambazo kamwe hazitatambuliwa . 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...