Meneja Masoko wa Mikono Business Consult Bi. Nestoria Simon (kulia) akimuelezea Bi .Anna Machanga,kuhusu faida ya moja ya vitabu vinavyopatikana katika banda lao,Katika maonesho ya Vodacom Elimu Expo yanayofanyika kwa siku tatu katika viwanja vya posta kijitonyama jijini Dar es salaam.
Baadhi ya wanafunzi wa shule ya Sekondari ya wasichana ya Premier iliyopo Bagamoyo Mkoa wa Pwani, wakifanya majarabio ya kuchanganya kemikali katika banda la shule yao katika maonesho ya Vodacom Elimu Expo yanayofanyika kwa siku tatu katika viwanja vya posta kijitonyama jijini Dar es salaam.
Meneja Matukio wa kampuni ya T- MARC Bi. Dorris Chalambo,akizungumza na waandishi wa habari kuhusu pedi zilizozinduliwa na kampuni hiyo kwa kushirikiana na Vodacom Foundation.Pedi hizo zinapatikana katika banda la kampuni hiyo kwenye maonesho ya Vodacom Elimu Expo yanayofanyika kwa siku tatu katika viwanja vya posta kijitonyama jijini Dar es salaam.
Waandishi wa habari wakimfanyia mahojiano Meneja Matukio wa kampuni ya T- MARC Bi.Dorris Chalambo, maonesho ya Vodacom Elimu Expo yanayofanyika kwa siku tatu katika viwanja vya posta kijitonyama jijini Dar es salaam,kuhusu na matumizi sahihi ya pedi zilizozinduliwa hivi karibuni na kampuni hiyo kwa ushirikiano na Vodacom Foundation,Anaeshuhudia kulia ni Mkuu wa Idara ya kusadia jamii(Vodacom Foundation)Yessaya Mwakifulefule.Maonesho hayo yanafanyika katika viwanja vya posta.
Mwanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Green Acres Innocent Maro (kushoto)akiwaelezea wanafunzi wa shule ya sekondari ya wasichana Premier ya Bagamoyo, kuhusu mafunzo yanayopatikana shuleni kwao kwa gharamaa nafuu.,wanafunzi hao walifika katika maonesho ya Vodacom Elimu Expo yanayofanyika kwa siku tatu katika viwanja vya posta kijitonyama jijini Dar es salaam.
Well done Premier Girls Secondary School.... thanks to Elimu Expo 2013, Michuzi na vyombo vya habari kwa support.
ReplyDelete