Waheshimiwa Mawaziri wa Tanzania walioshiriki katika Mkutano wa Kumi wa Baraza la Mawaziri wa Sekta ya Miundombinu Mawasiliano na Hali ya Hewa uliofanyika katika Hoteli ya Sports View jijini Kigali Rwanda tarehe 23 Agosti, 2013 wakifuatilia kwa Makini Mkutano huo. Kutoka kushoto ni Mheshimiwa Janeth Mbene Naibu Waziri wa Fedha akifuatiwa na Mheshimiwa Charles Tizeba Waziri wa Uchukuzi, kati kati ni   Mheshimiwa Aggrey Mwanri Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, akifuatiwa  na Mheshimiwa Gerson Rwenge Naibu Waziri wa Ujenzi na wa mwisho ni   Bwana John Mngodo aliyekuwa  Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Uchukuzi ambaye kwa sasa amehamishiwa Wizara ya Mwasiliano Sayansi na Technolojia.
Naibu Waziri wa Ukukuzi Mheshimiwa Charles Tizeba (kulia, aliyesimama) akjiandaa kutia saini itifaki ya Afrika Mashariki ya TEHAMA (Protocol for ICT network) na Sera ya Afrika Mashariki ya taarifa za hali ya Hewa (EAC Meteorological Data Policy). Wanaofuata ni Mawaziri wa Miundombinu kutoa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki pia wakisaini itifaki na Sera husika.
 Mkutano wa Kumi wa Baraza la Mawaziri wa Sekta ya Uchukuzi, Mawasiliano na Hali ya Hewa uliofanyika katika Hoteli ya Sports View Jijini Kigali Rwanda tarehe 23 Agosti, 2013, umemalizika

Mkutano huo ulihudhuriwa na Mheshimiwa Janeth Mbene Naibu Waziri wa Fedha  Mheshimiwa Charles Tizeba, Naibu Waziri wa Uchukuzi, MheshimiwaAggrey Mwanri Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Mheshimiwa Gerson Rwenge Naibu Waziri wa Ujenzi kutoka Tanzania

Katika Hotuba za ufunguzi Wakuu wa Msafara kutoka Nchi Wanachama walisisitiza uharakishaji wa utekelezaji wa Miradi ya kipaumbele iliyoanishwa na Wakuu wa Nchi Wanachama katika Retreat yao ya pili iliyofanyika Jijini Nairobi mwezi Novemba, 2012 iliyohusu Ufadhili na Uendelezaji wa Miundombinu.

Aidha Mkutano huo ulipokea taarifa ya utekelezaji wa Miradi na programu mbali mbali inayotekelezwa katika Nchi Wanachama. Katika kikao hicho ilielezwa kuwa ujenzi wa Vituo vya pamoja Mipakani uko katika hatua mbali mbali za ujenzi na kwa upande wa Vituo vya Namanga na Holili ujenzi unakaribia kukamilika na vituo hivyo vinategemewa kufunguliwa rasmi wakati wa Mkutano wa Wakuu wa Nchi wanachama utakaofanyika mwezi April, 2014.

Kukamilika kwa vituo hivyo kutawezesha na kuharakisha usafiri na usafirishaji wa mizigo miongoni mwa Nchi Wanachama kwa kuwezesha ukaguzi kufanyika upande mmoja wa mpaka na hivyo kuharakisha ufanyaji wa biashara.


Mkutano huo ulishuhudia mamlaka husika kutia saini Mkataba wa Makubaliano wa utafutaji na Uokoaji (Memorandum of Understanding on Search and Rescue), itifaki ya Afrika Mashariki ya TEHAMA (Protocol for ICT net work) na Sera ya Afrika Mashariki ya taarifa za hali ya Hewa (EAC Meteorological Data Policy).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...