Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Mhandisi Omar Chambo akitoa maelezo ya awali kabla ya kumkaribisha Waziri wa Uchukuzi, Dkt Harrison Mwakyembe(hayupo pichani) kufungua mkutano wa kwanza wa kamati ya Uendeshaji  ya Matokeo makubwa sasa katika sekta ya Uchukuzi, leo katika ukumbi Mikutano wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam.
 Wajumbe wa kamati ya Uendeshaji ya Matokeo Makubwa sasa (Big Result Now) ya sekta ya Uchukuzi wakimsikiliza Waziri wa Uchukuzi, Dkt. Harrison Mwakyembe(hayupo pichani), wakati Waziri huyo alipofungua mkutano wa kwanza wa kamati hiyo leo  katika ukumbi wa Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Uchukuzi, Dkt. Harrison Mwakyembe (wa pili kutoka kulia), akisisitiza jambo wakati wa mkutano wa kwanza uliowakutanisha wajumbe wa kamati ya uendeshaji ya Matokeo makubwa sasa(Big Result Now) kwa sekta ya Uchukuzi, wakati alipokutana na kamati hiyo leo mchana katika ukumbi wa Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam. Kulia kwa Waziri Mwakyembe ni Naibu Waziri wa Wizara ya Ujenzi, Gerson Lwenge. Kushoto kwa Waziri Mwakyembe ni Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Kusimamia utekelezaji wa Matokeo makubwa sasa iliyopo chini ya Ofisi y Rais, Bw. Omar Issa.
 Mratibu wa Miradi iliyo kwenye mpango wa Matokeo makubwa sasa katika sekta ya Uchukuzi, Bw. Aunyisa Meena akifafanua jambo wakati wa ufunguzi wa mkutano wa kwanza wa kamati ya Uendeshaji katika sekta ya Uchukuzi, leo mchana.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hodhi ya Rasilimali za Reli(RAHCO), Mhandisi Benhadard Tito akifafanua hatua iliyofikiwa kwenye miradi ambayo iko kwenye Mpango wa matokeo makubwa sasa katika sekta ya uchukuzi, wakati wa mkutano wa kwanza wa kamati ya uendeshaji katika sekta ya Uchukuzi,uliofanyika leo mchana katika ukumbi wa Julius Nyerere,jijini Dar es Salaam. PICHA NA KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINII UCHUKUZI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...