Mwenyekiti wa CCM Mkoa  wa Lindi ambae pia ni Mwenyekiti wa Wenyeviti wa CCM wa Mikoa,Ally Mohamedi Mtopa
 Kikundi cha ngoma cha Kiwalala kikitumbuiza katika maonyesho hayo
 Jengo la Maonesho ya Nane Nane
 Kutoka kushoto....Waziri wa Tamisemi, Mhe HawGhasia Mwenyekiti wa Taso kanda ya kusini,Waziri wa Katiba na Sheria Mhe Mathias Chikawe (Mgeni Rasmi) Mkuu wa mkoa wa Lindi na Mkuu wa wilaya ya Lindi
 Wakuu wa wilaya za mkoa wa Lindi na Mtwara
Washindi wa jumla maonesho ya nane nane wakisherehekea
-------------------
Na Abdulaziz Video
SERIKALI imetakiwa kutekeleza agizo lililotolewa na Chama cha mapinduzi (CCM) la kuwalipa fedha zilizobaki wakulima wa korosho kanda ya kusini,inayojumuisha mikoa ya Lindi na Mtwara,ili kuondoa malalamiko yasiyo ya msingi zidi ya Serikali yao. 
Akitoa salamu za CCM,Mwenyekiti wa Mkoa ambae pia ni Mwenyekiti wa Wenyeviti wa CCM wa Mikoa,Ally Mohamedi wakati wa ufungaji wa maonesho ya 4 ya wakulima nanenane,kanda ya kusini yaliyofanyika viwanja vya ngongo katika Manispaa ya Lindi,alisema anashangazwa kuona Serikali ikishikwa na kigugumizi katika kutekeleza agizo iliyopewa Na Chama chake kuingilia kati mgogoro wa wakulima wa korosho,ikiwemo kuwalipa fedha zao zilizosalia baada ya zao hilo kukosa soko. 
“Chama kilishatoa agizo kwa kuitaka Serikali kuingilia kati ikiwa ni pamoja na kuwalipa wakulima wa korosho fedha zao zilizobakia Baada ya pilikapilika na kupiga kelele juu ya masuala ya korosho,Chama kilinituma nikaonane na waziri mkuu,kumuulizia lile agizo April 23 mwaka huu,la kuwalipa wakulima wa korosho Sh,600/-limefikia wapi?,,,,,,lakini kwa bahati mbaya sikupata nafasi ya kuonana nae kutokana na kuwa katika ziara za kiserikali sasa serikali ipo hapa nyie mawaziri ndio serikali mnamuogopa nani?”Alisema Mtopa. 
 Akasema kitendo cha Serikali kuendelea kulifumbia macho agizo lililotolewa na Chama chake,juu ya malalamiko ya wananchi, kinawanyong’onyesha na kuwakatisha tama wakulima wakiwemo wa korosho. Pia,mwenyekiti huyo wa Chama mkoani Lindi,alisema inakuwaje Bodi ya korosho au vyama vya msingi vya ushirika wa ununuzi wa mazao vinakuwa na nguvu kuishinda Serikali katika kutatua kero za wananchi wake. 
 Mtopa amesisitiza kwa kutoa angalizo,iwapo Serikali hawatalipa fedha kwa wakulima hao wa korosho,kuna hatari ya wananchi kutoendelea kukiamini tena Chama hicho katika chaguzi zijazo ikiwemo katika utekelezaji wa Stakabadhi ghalani. 
 Naye,waziri wa katiba na Sheria,Mathias Chikawe,ambaye alikuwa ni mgeni rasmi katika ufungaji wa maonesho hayo ya nanenane,amehaidi kukutana na mawaziri wenzake kwa lengo kuyazungumza,kabla ya kukutana na waziri mkuu. 
"Naahidi kulifanyia kazi pamoja na mawaziri wenzangu hata hivyo tutapiga debe pia ili Nane nane mwakani Kitaifa iwe Viwanja vya Ngongo kwa mara ya kwanza kanda ya kusini Mwanzoni mwa mwaka huu,wakulima wa korosho wilaya tatu kati ya tano za mkoa wa Lindi, ambazo ni Liwale, Ruangwa na Kilwa,walifanya vurugu ikiwemo kuharibu mali za viongozi wakiwemo wanasiasa na vyama vya msingi vya ushirika.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Huyu Waziri jina la baba ni Ghasia sio Gasia kama wanavyotamka wasomaji wa habari maredioni na ma-tv-ini. Ghasia ni neno la Kiswahili ambalo maana yake ni kelele. Gasia sio neno la Kiswahili.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...